Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 HABARI KUU: JE, DINI INAWEZA KUTEGEMEKA?

Kwa Nini Tuchunguze Dini?

Kwa Nini Tuchunguze Dini?

Tuseme unahitaji kufanyiwa upasuaji kwa sababu una ugonjwa hatari. Ungehitaji kuwa na uhakika na daktari atakayekufanyia upasuaji, kwa sababu maisha yako yanamtegemea. Lingekuwa jambo la busara kuchunguza uzoefu wake, sivyo?

Vivyo hivyo, ni jambo la busara kuchunguza dini kwa uangalifu. Ikiwa wewe ni mfuasi wa dini fulani, kwa kweli uhusiano wako na Mungu unategemea dini hiyo. Hilo linahusisha tumaini lako la kuishi milele.

Yesu aliweka kiwango cha kutusaidia kuchunguza dini. Alisema: “Kila mti hujulikana kwa matunda yake.” (Luka 6:44) Kwa mfano, unapochunguza dini fulani, jiulize, inatokeza matunda ya aina gani? Je, viongozi wa dini hiyo wanasisitiza sana kukusanya pesa? Je, wafuasi wake wanafuata kanuni za Biblia kuhusu vita na maadili? Mwishowe, je, kuna dini yoyote inayotegemeka? Tunakuomba uchunguze makala zifuatazo.

“Kila mti hujulikana kwa matunda yake.”—Luka 6:44