Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 19

Je, Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli?

Je, Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli?

Sisi Mashahidi wa Yehova tunaamini kwamba sisi ni Wakristo wa kweli. Kwa nini? Chunguza msingi wa mambo tunayoamini, jina letu la kipekee, na upendo tulio nao miongoni mwetu.

1. Ni nini msingi wa imani ya Mashahidi wa Yehova?

Yesu alisema “neno [la Mungu] ni kweli.” (Yohana 17:17) Kama Yesu, sikuzote Mashahidi wa Yehova wametegemea Neno la Mungu kuwa msingi wa imani yao. Fikiria historia ya Mashahidi wa Yehova. Mwishoni mwa karne ya 19, kikundi cha wanafunzi wa Biblia kilianza kuichunguza Biblia kwa makini. Mambo waliyoamini yalitegemea Neno la Mungu, hata yalipotofautiana na mafundisho ya makanisa mengine. Kisha wakaanza kuzungumza na watu wengine kuhusu kweli hizo za Biblia. a

2. Kwa nini tunaitwa Mashahidi wa Yehova?

Yehova anasema kwamba wale wanaomwabudu ni Mashahidi wake kwa sababu wanatangaza ukweli kumhusu. (Waebrania 11:4–12:1) Kwa mfano, nyakati za kale Mungu aliwaambia hivi watu wake: “Ninyi ni mashahidi wangu.” (Soma Isaya 43:10.) Yesu anaitwa “Shahidi Mwaminifu.” (Ufunuo 1:5) Hivyo, kuanzia mwaka wa 1931, tuliamua kuitwa Mashahidi wa Yehova. Tunajivunia kuitwa kwa jina hilo.

3. Mashahidi wa Yehova wanaigaje upendo wa Yesu?

Yesu aliwapenda sana wanafunzi wake hivi kwamba walikuwa kama familia yake. (Soma Marko 3:35.) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova ni familia ya ulimwenguni pote yenye umoja. Ndiyo sababu tunaitana ndugu na dada. (Filemoni 1, 2) Vilevile tunatii amri hii: “Upendeni ushirika mzima wa akina ndugu.” (1 Petro 2:17) Mashahidi wa Yehova wanaonyesha upendo katika njia nyingi, kwa mfano, tunawasaidia waamini wenzetu ulimwenguni pote wanapohitaji msaada.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze kuhusu historia ya Mashahidi wa Yehova, na uone uthibitisho wa kwamba sisi ni Wakristo wa kweli.

Imani ya Wakristo wa kweli inategemea Biblia nao huwafundisha wengine mambo wanayojifunza

4. Biblia ndiyo msingi wa imani yetu

Yehova alitabiri kwamba kweli za Biblia zingefunuliwa. Soma Danieli 12:4 na maelezo ya chini, kisha mzungumzie swali hili:

  • Watu wa Mungu wangepata nini “kwa wingi” kwa kuendelea kuchunguza Biblia?

Chunguza jinsi kikundi cha wanafunzi wa Biblia, kutia ndani Charles Russell, walivyojifunza Neno la Mungu. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Katika video hiyo, Charles Russell na wanafunzi wenzake wa Biblia walitumia njia gani kujifunza Biblia?

Je wajua?

Nyakati nyingine, tunarekebisha baadhi ya mambo tunayoamini. Kwa nini? Kama vile vitu vinavyoonekana wazi zaidi jua linapochomoza na kuzidi kung’aa, ndivyo Mungu anavyotufunulia Neno lake hatua kwa hatua. (Soma Methali 4:18.) Hivyo, ingawa Biblia haibadiliki, tunarekebisha mambo tunayoamini kadiri tunavyozidi kuielewa Biblia.

5. Tunaishi kulingana na jina letu

Kwa nini tulichagua kuitwa Mashahidi wa Yehova? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Kwa nini jina Mashahidi wa Yehova linafaa?

Kwa nini Yehova amechagua wanadamu wawe mashahidi wake? Kwa sababu uwongo mwingi umeenezwa kumhusu, hivyo anataka wamtambulishe kuwa Mungu wa kweli. Fikiria mafundisho mawili ya uwongo kumhusu.

Baadhi ya dini huwafundisha wafuasi wao kwamba Mungu anataka watumie sanamu katika ibada. Je, fundisho hilo ni la kweli? Soma Mambo ya Walawi 26:1, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ukweli ni nini? Yehova ana maoni gani kuhusu kutumia sanamu?

Baadhi ya viongozi wa dini hufundisha kwamba Yesu ni Mungu. Je, fundisho hilo ni la kweli? Soma Yohana 20:17, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ukweli ni nini? Je, Mungu na Yesu ni mtu yuleyule?

  • Unahisije unapojua kwamba Yehova amewatuma Mashahidi wake ili wahubiri ukweli kumhusu yeye na Mwana wake?

6. Tunapendana

Biblia inasema Wakristo wanapaswa kuungana kama viungo mbalimbali katika mwili wa mwanadamu. Soma 1 Wakorintho 12:25, 26, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Wakristo wa kweli wanapaswa kufanya nini Wakristo wenzao wanapoteseka?

  • Umetambua jambo gani kuhusu upendo ulio miongoni mwa Mashahidi wa Yehova?

Mashahidi wa Yehova wanapoteseka katika sehemu moja ya dunia, Mashahidi wenzao ulimwenguni pote huchukua hatua haraka ili kuwasaidia. Ili uone mfano mmoja, onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Jitihada za Mashahidi wa Yehova za kutoa msaada zinathibitishaje kwamba wanapendana?

Wakristo wa kweli huwaonyesha upendo watu wanaohitaji msaada

WATU FULANI HUSEMA: “Mashahidi wa Yehova ni dini mpya.”

  • Yehova alianza lini kuwaita waabudu wake mashahidi?

MUHTASARI

Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli. Sisi ni familia ya waabudu walio ulimwenguni pote. Imani yetu inategemea Biblia na tunatangaza ukweli kumhusu Yehova.

Ungejibuje?

  • Kwa nini tulichagua kuitwa Mashahidi wa Yehova?

  • Tunaonyeshaje kwamba tunapendana?

  • Je, unafikiri Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Ona mfano mmoja wa jinsi Mashahidi wa Yehova walivyofunua mafundisho ya uwongo.

Watu wa Mungu Hulitukuza Jina Lake (7:08)

Pata majibu ya maswali ambayo huenda umejiuliza kuhusu Mashahidi wa Yehova.

“Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova” (habari zilizo kwenye mtandao)

Stephen alikuwa mhalifu aliyeongozwa na chuki. Ona jambo aliloona miongoni mwa Mashahidi wa Yehova lililomchochea kufanya mabadiliko.

“Maisha Yangu Yalizidi Kuwa Mabaya” (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2015)

a Gazeti letu kuu Mnara wa Mlinzi, limekuwa likitangaza kweli za Biblia tangu mwaka wa 1879.