Ufunuo kwa Yohana 1:1-20

  • Ufunuo kutoka kwa Mungu, kupitia Yesu (1-3)

  • Salamu kwa yale makutaniko saba (4-8)

    • “Mimi ndiye Alfa na Omega” (8)

  • Yohana katika siku ya Bwana kwa mwongozo wa roho (9-11)

  • Maono ya Yesu aliyetukuzwa (12-20)

1  Ufunuo* kupitia Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa+ ili kuwaonyesha watumwa wake+ mambo yanayopaswa kutukia hivi karibuni. Naye alimtuma malaika wake na kupitia yeye akautoa kwa ishara kwa mtumwa wake Yohana,+  aliyetoa ushahidi kuhusu neno ambalo Mungu alisema na kuhusu ushahidi ambao Yesu Kristo alitoa, ndiyo, kuhusu mambo yote aliyoyaona.  Mwenye furaha ni yule anayesoma kwa sauti na wale wanaosikia maneno ya unabii huu, na wanaoshika mambo yaliyoandikwa humo,+ kwa kuwa wakati uliowekwa uko karibu.  Yohana, kwa makutaniko saba+ yaliyo katika mkoa wa Asia: Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja,”+ na kutoka kwa zile roho saba+ zilizo mbele ya kiti chake cha ufalme,  na kutoka kwa Yesu Kristo, “Shahidi Mwaminifu,”+ “mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,”+ na “Mtawala wa wafalme wa dunia.”+ Yeye anayetupenda+ na aliyetuweka huru kutoka katika dhambi zetu kupitia damu yake mwenyewe+  naye alitufanya tuwe ufalme,+ makuhani+ kwa Mungu na Baba yake—ndiyo, na awe na utukufu na nguvu milele. Amina.  Tazama! Anakuja na mawingu,+ na kila jicho litamwona, na wale waliomchoma;* na makabila yote ya dunia yatajipigapiga kwa huzuni kwa sababu yake.+ Ndiyo, Amina.  “Mimi ndiye Alfa na Omega,”*+ asema Yehova* Mungu, “Yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja, Mweza-Yote.”+  Mimi Yohana, ndugu yenu na mshiriki pamoja nanyi katika dhiki+ na ufalme+ na uvumilivu+ katika ushirika na Yesu,+ nilikuwa katika kisiwa kinachoitwa Patmo kwa sababu ya kuzungumza kumhusu Mungu na kutoa ushahidi kumhusu Yesu. 10  Kwa mwongozo wa roho nilikuja kuwa katika siku ya Bwana, nami nikasikia nyuma yangu sauti yenye nguvu kama ya tarumbeta, 11  ikisema: “Yale unayoona, yaandike katika kitabu cha kukunjwa kisha uyatume kwa yale makutaniko saba: katika Efeso,+ katika Smirna,+ katika Pergamamu,+ katika Thiatira,+ katika Sardi,+ katika Filadelfia,+ na katika Laodikia.”+ 12  Nikageuka ili nimwone yule aliyekuwa akizungumza nami, nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,+ 13  na katikati ya vinara hivyo vya taa palikuwa na mtu kama mwana wa binadamu,+ aliyevaa vazi lililofika chini miguuni na kifuani alikuwa amevaa mshipi wa dhahabu. 14  Zaidi ya hayo, kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto,+ 15  na miguu yake ilikuwa kama shaba safi+ inapowaka katika tanuru, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi. 16  Na kwenye mkono wake wa kuume kulikuwa na nyota saba,+ na kutoka katika kinywa chake upanga mkali, mrefu, wenye makali pande mbili+ ulikuwa umechomoza, na sura yake ilikuwa* kama jua linapong’aa kabisa.+ 17  Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kana kwamba nimekufa. Naye akaweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope. Mimi ndiye wa Kwanza+ na wa Mwisho,+ 18  na aliye hai,+ nami nilikufa,+ lakini tazama! ninaishi milele na milele,+ nami nina funguo za kifo na za Kaburi.*+ 19  Kwa hiyo andika mambo uliyoona, na mambo yaliyopo, na mambo yatakayotukia baada ya haya. 20  Kuhusu siri takatifu ya zile nyota saba ulizoona kwenye mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu: Zile nyota saba zinamaanisha wale malaika wa yale makutaniko saba, na vile vinara saba vya taa vinamaanisha yale makutaniko saba.+

Maelezo ya Chini

Au “Kufichua siri.”
Au “waliomdunga.”
Au “herufi A na Z.” Alfa ni herufi ya kwanza na Omega ni herufi ya mwisho katika alfabeti ya Kigiriki.
Au “uso wake ulikuwa.”
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.