Hamia kwenye habari

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumii Msalaba Katika Ibada?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumii Msalaba Katika Ibada?

 Watu wengi huona msalaba kuwa ishara inayowatambulisha Wakristo ulimwenguni pote. Ingawa Mashahidi wa Yehova ni Wakristo, hatutumii msalaba katika ibada yetu. Kwa nini?

 Sababu moja ni kwamba Biblia inaonyesha kwamba Yesu hakufa juu ya msalaba bali alikufa juu ya mti wa kawaida. Isitoshe, Biblia inawaonya vikali Wakristo ‘waikimbie ibada ya sanamu,’ na hilo linamaanisha wasitumie msalaba katika ibada.​— 1 Wakorintho 10:14; 1 Yohana 5:21.

 Jambo muhimu hata zaidi ni kwamba Yesu alisema hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.” (Yohana 13:34, 35) Kwa maneno hayo, Yesu alionyesha kwamba wafuasi wake wa kweli wangetambuliwa kwa upendo wao wenye kujidhabihu na si kwa msalaba au sanamu nyingine.