Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 10:1-33

  • Vielelezo vya kuonya kutokana na historia ya Israeli (1-13)

  • Onyo dhidi ya ibada ya sanamu (14-22)

    • Meza ya Yehova, meza ya roho waovu (21)

  • Uhuru na kuwafikiria wengine (23-33)

    • “Fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu” (31)

10  Basi akina ndugu, ninataka mjue kwamba mababu zetu wote walikuwa chini ya wingu+ na wote walipita katika bahari+  na wote walibatizwa katika Musa kupitia wingu na bahari,  na wote walikula chakula kilekile cha kiroho+  na wote walikunywa maji yaleyale ya kiroho.+ Kwa maana walikuwa wakinywa kutokana na mwamba wa kiroho uliowafuata, na mwamba huo ulimaanisha* Kristo.+  Hata hivyo, Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa maana waliangamizwa nyikani.+  Basi mambo hayo yalikuwa vielelezo kwetu, ili tusitamani mambo mabaya, kama wao walivyotamani.+  Wala tusiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyofanya; kama ilivyoandikwa: “Watu wakaketi ili wale na kunywa. Kisha wakasimama ili wajitumbuize.”+  Wala tusifanye uasherati,* kama baadhi yao walivyofanya uasherati,* na 23,000 kati yao wakaanguka kwa siku moja.+  Wala tusimjaribu Yehova,*+ kama baadhi yao walivyomjaribu, wakaangamizwa na nyoka.+ 10  Wala tusiwe wanung’unikaji,+ kama baadhi yao walivyonung’unika, wakaangamizwa na mwangamizaji.+ 11  Basi mambo hayo yaliwapata ili kuwa vielelezo, nayo yaliandikwa ili kuwa onyo kwetu sisi+ ambao tumefikiwa na miisho ya mifumo ya mambo. 12  Basi yule anayefikiri amesimama na ajihadhari asije akaanguka.+ 13  Hakuna majaribu ambayo yamewapata ninyi ila yale yaliyo ya kawaida kwa watu.+ Lakini Mungu ni mwaminifu, naye hatawaacha mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili,+ bali pamoja na majaribu hayo ataifanya pia njia ya kutokea ili mweze kuyavumilia.+ 14  Kwa hiyo, wapendwa wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.+ 15  Ninasema kana kwamba ni kwa watu wenye utambuzi; hukumuni wenyewe lile ninalosema. 16  Kikombe cha baraka ambacho tunabariki, je, si kushiriki katika damu ya Kristo?+ Mkate ambao tunamega, je, si kushiriki katika mwili wa Kristo?+ 17  Kwa sababu kuna mkate mmoja, sisi, ingawa tuko wengi, ni mwili mmoja,+ kwa maana sote tunakula mkate huo mmoja. 18  Tazameni Israeli kwa njia ya kimwili: Je, wale wanaokula dhabihu si washiriki pamoja na madhabahu?+ 19  Basi, niseme nini? Je, kile kilichotolewa dhabihu kwa sanamu ni kitu, au je, sanamu ni kitu? 20  Hapana; bali ninasema kwamba vitu ambavyo mataifa huvitoa dhabihu, wao huvitoa dhabihu kwa roho waovu, si kwa Mungu;+ nami sitaki muwe washiriki pamoja na roho waovu.+ 21  Hamwezi kuwa mkinywa kikombe cha Yehova* na kikombe cha roho waovu; hamwezi kuwa mkishiriki “meza ya Yehova”*+ na meza ya roho waovu. 22  Au je, ‘tunamchochea Yehova* kuwa na wivu’?+ Je, sisi tuna nguvu zaidi kuliko yeye? 23  Mambo yote ni halali,* lakini si mambo yote yaliyo na faida. Mambo yote ni halali, lakini si mambo yote yanayojenga.+ 24  Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali faida ya yule mtu mwingine.+ 25  Kuleni chochote kinachouzwa katika soko la nyama, bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu, 26  kwa maana “dunia na vyote vilivyomo ni vya Yehova.”*+ 27  Mtu asiyeamini akiwaalika nanyi mtake kwenda, kuleni chochote kinachowekwa mbele yenu, bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu. 28  Lakini yeyote akiwaambia, “Hiki ni kitu kilichotolewa katika dhabihu,” msile kwa sababu ya yule aliyewaambia na kwa sababu ya dhamiri.+ 29  Simaanishi dhamiri yako mwenyewe, bali ya yule mtu mwingine. Kwa maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?+ 30  Ikiwa ninakula nikiwa na shukrani, kwa nini nitukanwe juu ya kile ninachotolea shukrani?+ 31  Kwa hiyo, iwe mnakula au mnakunywa au mnafanya jambo lingine lolote, fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu.+ 32  Epukeni kuwa vikwazo kwa Wayahudi na vilevile kwa Wagiriki na kwa kutaniko la Mungu,+ 33  kama vile ninavyojaribu kuwapendeza watu wote katika mambo yote, bila kutafuta faida yangu mwenyewe,+ bali faida ya walio wengi, ili wapate kuokolewa.+

Maelezo ya Chini

Au “ulikuwa.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “yanakubalika.”