Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JW LIBRARY

Pakua na Utumie Biblia​—iOS

Pakua na Utumie Biblia​—iOS

Kusoma na kujifunza Biblia ni sehemu kuu ya JW Library.

Fuata maelekezo yafuatayo kupakua na kutumia Biblia:

 Pakua Biblia

Unaweza kupakua tafsiri mbalimbali za Biblia ili usome na kujifunza hata unapozima intaneti.

  • Bonyeza tabo ya Biblia kuona orodha ya vitabu vya Biblia.

  • Bofya kitufe cha Lugha ili uone orodha ya Biblia zilizopo. Tafsiri za lugha unazotumia mara nyingi zinapangwa juu kwenye orodha hiyo. Unaweza pia kutafuta Biblia kwenye orodha hiyo kwa kuandika jina la lugha au Biblia hiyo. Kwa mfano, andika “int” ili upate Biblia ya Kingdom Interlinear ya Kiingereza, au “port” ili kupata Biblia zote za Kireno.

  • Biblia ambazo bado hazijapakuliwa zina alama ya wingu. Bofya Biblia ili uipakue. Biblia inapopakuliwa kwenye kifaa chako, alama ya wingu hutoweka. Bofya Biblia hiyo ili uisome.

Usipoona tafsiri ya Biblia unayotaka, tafadhali tafuta baadaye. Tafsiri nyingine zitaongezwa kadiri zinavyopatikana.

 Ondoa Biblia

Ikiwa huhitaji tafsiri fulani ya Biblia au ungependa kupata nafasi zaidi kwenye kifaa chako, unaweza kuifuta.

Bofya tabo ya Biblia, kisha bonyeza kitufe cha Lugha ili kufungua orodha ya Biblia. Tafuta Biblia unayotaka kufuta, kisha bofya Ondoa.

 Sasisha Biblia

Mara kwa mara, huenda Biblia uliyopakua ikarekebishwa.

Biblia iliyorekebishwa huwa na alama ya vishale. Unapobofya Biblia hiyo, utaona ujumbe kwamba Biblia hiyo imerekebishwa. Bofya Pakua ili uisasishe, au bofya Baadaye ili uendelee kusoma tafsiri ileile.

Sehemu hizo mbalimbali zilipatikana Februari 2015 kwenye JW Library toleo la 1.4, ambalo linafanya kazi vizuri kwenye vifaa vinavyotumia mfumo wa iOS 6.0 au wa karibuni zaidi. Ikiwa hauoni mambo haya, tafadhali fuata mwelekezo kwenye makala “Anza Kutumia JW Library​—iOS,” kwenye Pata Habari za Karibuni Zaidi.