Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JW LIBRARY

Tumia Historia​—iOS

Tumia Historia​—iOS

JW Library inahifadhi historia ya makala na sura za Biblia unazosoma. Hilo linaweza kuwa na faida, kwa mfano, unapotaka kurudi kwenye andiko ulilokuwa umesoma mapema.

Fuata maelekezo yafuatayo ili kutumia Historia:

 Fungua Orodha ya Historia

Bofya na ukandamize tabo ya Biblia ili kuona orodha ya maandiko ambayo umesoma karibuni. Bonyeza andiko kwenye orodha ya historia ili kufungua andiko hilo.

Bonyeza kwa muda mrefu tabo ya Machapisho ili kuona orodha ya habari zilizo kwenye machapisho uliyosoma hivi karibuni. Bofya makala unayotaka katika orodha ya historia ili uisome tena.

 Futa Historia

Bofya na ukandamize tabo ya Biblia au Machapisho ili ufungue orodha ya historia. Bofya kitufe cha Futa ili ufute kila kitu kwenye orodha hiyo.

Sehemu hizo mbalimbali zilipatikana Mei 2015 kwenye JW Library toleo la 1.2, ambalo linafanya kazi vizuri kwenye vifaa vinavyotumia mfumo wa iOS 6.0 au wa karibuni zaidi. Ikiwa hauoni mambo haya, tafadhali fuata mwelekezo kwenye makala “Anza Kutumia JW Library​—iOS,” kwenye Pata Habari za Karibuni Zaidi.