Ona video zinazopatikana

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Kupambana na Matatizo ya Feza?

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Kupambana na Matatizo ya Feza?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Kanuni ine zinazofuata zinaweza kukusaidia kuhusiana na matatizo ya feza na madeni:

  1.   Panga namna utatumia feza zako. ‘Mipango ya mwenye bidii bila shaka huleta faida, lakini kila mutu anayetenda haraka-haraka bila shaka huuelekea uhitaji.’ (Methali 21:5) Usinunue kitu haraka kwa sababu tu kimepunguzwa bei. Fanya bajeti ao namna ya kupangia matumizi ya feza zako, na uiheshimu mupango huo.

  2.   Epuka madeni yasiyo ya lazima. ‘Mukopaji ni mutumishi wa mutu anayemukopesha.’ (Methali 22:7) Ikiwa tayari una madeni na unashindwa kuyalipa, jaribu kuzungumuza na wale waliokukopesha, waombe wakuongezee siku ao wapunguze faida unazoombwa kurudisha. Usichoke kuzungumuza nao. Tenda kama yule mutu anayezungumuziwa katika Methali 6:1-5: “Ujinyenyekeze, na sihi jirani yako. Usiache macho yako kupata usingizi, wala kope zako kusinzia.” (La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Ikiwa hawakubali kwa mara ya kwanza, endelea kuwaomba wakuongezee siku ao wakupunguzie faida.

  3.   Usiwe mutumwa wa feza. ‘Mutu bahili [muchoyo] hukimbilia mali, wala hajui kwamba ufukara [umaskini] utamujia.’ (Methali 28:22, Biblia Habari Njema) Tamaa na pupa vinaweza kumuletea mutu matatizo mengi ya feza na kumufanya akose wakati kwa ajili ya mambo ya kiroho.

  4.   Tosheka na vitu vya lazima. ‘Kwa hiyo, tukiwa na chakula na kitu cha kujifunika, tutarizika na vitu hivyo.’ (1 Timotheo 6:8) Furaha katika maisha na kutosheka havitokane na feza. Kati ya watu wenye furaha zaidi duniani, kuna wale ambao hawana feza nyingi. Wanatosheka na upendo wanaonyeshwa na familia na marafiki na uhusiano wao pamoja na Mungu.​—Methali 15:17; 1 Petro 5:6, 7.