Ya Kwanza kwa Timoteo 6:1-21

  • Watumwa waheshimie mabwana wao (1, 2)

  • Walimu wa uongo na kupenda feza (3-10)

  • Maagizo kwa ajili ya mutu wa Mungu (11-16)

  • Kuwa tajiri katika matendo ya muzuri (17-19)

  • Linda mambo yenye ulipewa (20, 21)

6  Wale wote wenye kuwa chini ya nira ya utumwa waendelee kuona mabwana wao kuwa wanastahili heshima kamili,+ ili watu wasiseme mubaya+ hata siku moja juu ya jina la Mungu na fundisho lake.  Zaidi ya hayo, wale wenye kuwa na mabwana wenye kuamini, wasiwazarau kwa sababu wao ni ndugu. Lakini, wanapaswa kuwatumikia kwa utayari zaidi, kwa sababu wale wenye wanafaidika na utumishi wao muzuri ni waamini wenzao na wapendwa. Endelea kufundisha mambo haya na kutoa vitia-moyo hivi.  Kama mutu yeyote anafundisha fundisho lingine na hakubaliane na agizo lenye faida,*+ lenye kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, ao hakubaliane na fundisho lenye kupatana na ushikamanifu kwa Mungu,+  yeye anajivuna kwa kiburi na haelewe kitu.+ Anapenda sana* ubishi na mashindano juu ya maneno.+ Mambo hayo yanaleta wivu, mizozo, uchongezi,* na kuwazia wengine mubaya,  mabishano yenye kuendelea juu ya mambo ya kidogo-kidogo, yenye kufanywa na watu wenye wameharibika katika akili+ na hawaelewe tena ile kweli, na wanawaza kama ushikamanifu kwa Mungu ni njia ya kupata faida.+  Hakika, kuko faida kubwa katika ushikamanifu kwa Mungu+ pamoja na kutosheka.  Kwa maana hatukuleta kitu katika ulimwengu, na hatuwezi kutoka na kitu.+  Basi, kama tuko na chakula* na nguo,* tutatosheka na vitu hivyo.+  Lakini wale wenye wameazimia kuwa matajiri wanaanguka katika jaribu na mutego+ na tamaa nyingi za upumbavu na zenye kuumiza, zenye zinaingiza watu katika uharibifu na maangamizi.+ 10  Kwa maana kupenda feza ni chanzo cha mambo ya mubaya ya namna zote, na kwa kujikaza kufikia upendo huo, watu wengine wamepotoshwa kutoka kwenye imani, na wamejitoboa wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.+ 11  Hata hivyo, wewe, Ee mutu wa Mungu, kimbia mambo hayo. Lakini, fuatilia haki, ushikamanifu kwa Mungu, imani, upendo, uvumilivu, na upole.+ 12  Pigana pigano la muzuri la imani; shika sana ule uzima wa milele wenye wewe uliitiwa na ukatoa tangazo la muzuri la waziwazi mbele ya mashahidi wengi. 13  Mbele ya Mungu, mwenye analinda vitu vyote viendelee kuishi, na Kristo Yesu, mwenye akiwa shahidi alitoa tangazo la muzuri la waziwazi mbele ya Pontio Pilato,+ mimi ninakupatia maagizo 14  kwamba ushike amri na ubakie bila doa na bila kulaumiwa mupaka wakati wa kufunuliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo,+ 15  kwenye ule mwenye furaha na yeye pekee ambaye ni Bwana Mwenye Uwezo ataonyesha katika wakati wake wenye uliwekwa. Yeye ndiye Mufalme wa wale wenye kutawala wakiwa wafalme na Bwana wa wale wenye kutawala wakiwa mabwana,+ 16  yeye peke yake mwenye hawezi kufa,+ mwenye anaishi katika mwangaza wenye hauwezi kufikiwa,+ mwenye hakuna mwanadamu mwenye amemuona ao mwenye anaweza kumuona.+ Kwake yeye kukuwe heshima na nguvu ya milele. Amina. 17  Agiza* wale wenye kuwa matajiri katika mupangilio wa mambo* wa sasa wasikuwe na majivuno,* wala wasiweke tumaini lao katika utajiri wenye hauko hakika,+ lakini katika Mungu, mwenye anatupatia kwa wingi vitu vyote vyenye tunafurahia.+ 18  Uwaambie watende mema, wakuwe matajiri katika matendo ya muzuri, wakuwe wakarimu,* tayari kushiriki na wengine;+ 19  kwa kufanya vile, watajiwekea kwa usalama hazina ya musingi muzuri kwa ajili ya wakati wenye kuja,+ ili washike sana uzima wa kwelikweli.+ 20  Timoteo, linda yote yenye ulipewa,+ ujiepushe na maneno yenye hayana maana yenye yanachafua mambo matakatifu, pia ujiepushe na maneno yenye kupingana ya ule wenye unaitwa kwa uongo “ujuzi.”+ 21  Kwa kujisifia ujuzi huo, wengine wamegeuka na kuacha imani. Fazili zenye hazistahiliwe zikuwe pamoja na ninyi.

Maelezo ya Chini

Ao “lenye kujenga afya.”
Ao “Anapenda kwa njia yenye haiko sawa.”
Ao “matusi.”
Ao “riziki.”
Ao “makao.” Tnn., “kitu cha kujifunika.”
Ao “Amuru.”
Ao “wasitake makubwa.”
Ao “mufumo wa mambo.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “wakuwe tayari kutoa.”