Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Juu ya Kuishi Pamoja Mbele ya Kufunga Ndoa?

Biblia Inasema Nini Juu ya Kuishi Pamoja Mbele ya Kufunga Ndoa?

Jibu ya Biblia

 Biblia inasema kama Mungu anapenda watu ‘wajiepushe na uasherati.’ (1 Watesalonike 4:3) Wakati neno uasherati inatumiwa mu Biblia inamaanisha uzinifu, ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke, na ngono kati ya mwanaume na mwanamunke wenye hawayaoana.

 Juu ya nini Mungu anapenda mwanamuke na mwanaume waoane mbele waanze kuishi pamoja?

  •   Mungu njo alianzisha ndoa alifanya vile wakati aliunganisha mwanaume na mwanamuke wa kwanza. (Mwanzo 2:22-24) Alipenda mwanamuke na mwanaume waoane na washikamane maisha yao yote, hapana kwa wakati kidogo tu.

  •   Mungu anajua nini njo inaweza kuletea wanadamu furaha. Wakati Mungu alianzisha ndoa, alipenda iunganishe mwanaume na mwanamuke maisha yao yote. Ndoa ni mupango wenye unalinda na kuletea faida kila mutu mu familia. Kwa mufano, mutu mwenye anatengeneza kitu anatoaka maagizo juu ya namna ya kuiunganisha muzuri. Vilevile, Mungu anatuambia mambo ya kufanya juu tukuwe na familia yenye furaha. Watu wenye wanafuata sheria za Mungu wanapataka faida.​—Isaya 48:17, 18.

    Mutu mwenye anatengeneza kitu anatoaka maagizo juu ya namna ya kuiunganisha muzuri. Vilevile, Mungu anatuambia mambo ya kufanya juu tukuwe na familia yenye furaha

  •   Wale wenye wanafanya ngono mbele waoane wanapataka magumu ya mingi. Kwa mufano, mimba yenye haikutazamiwa, magonjwa ya kuambuiza kupitia ngono, na huzuni ya mingi sana.

  •   Mungu alipatia mwanaume na mwanamuke zawadi ya ngono na ile inawasaidia kuzaa watoto. Mungu anaona uzima kuwa takatifu; na uwezo wa kuzaa watoto ni zawadi ya maana sana. Mungu anapenda mutu afanye tu ngono na bibi au bwana yake. Wakati tunamutii, tunaonyesha kama tunaheshimia ile zawadi.​—Waebrania 13:4.

 Ni muzuri kuanza kuishi pamoja mbele ya kufunga ndoa juu ya kuona kama munapatana?

 Juu ndoa ikuwe na furaha, haiko lazima watu waishi kwanza pamoja kwa wakati fulani mbele ya kuoana. Lakini ndoa inakuwa nguvu wakati bibi na bwana wanashikamana kabisa na wanatumika pamoja juu ya kumaliza magumu yao. Kuoana inafanyaka washikamane sana juu wanafanyaka naziri kama watabakia pamoja.​—Matayo 19:6.

 Bibi na bwana wanaweza kufanya nini juu ndoa yao ikuwe na furaha?

 Hakuna ndoa yenye haikuwake na magumu. lakini bibi na bwana wanaweza kuwa na furaha kama wanatumikisha mashauri ya Biblia. Ona mashauri fulani.