Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kufanya Ngono Mbele ya Kufunga Ndoa

Kufanya Ngono Mbele ya Kufunga Ndoa

MAONI YA BIBLIA

Kufanya Ngono Mbele Ya Kufunga Ndoa Kufanya Ngono Mbele Ya Kufunga Ndoa

Ni vibaya kufanya ngono mbele ya kufunga ndoa?

‘Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, . . . kwamba mujiepushe na uasherati.’​—1 Wathesalonike 4:3.

MAMBO AMBAYO WATU WANASEMA Watu wa desturi fulani wanakubali ngono kati ya watu wazima ambao hawaoane ikiwa wanapatana. Katika maeneo fulani ni jambo lenye kukubalika vijana ambao hawaoane kuwa na aina fulani ya uhusiano wa kingono kati yao.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA Biblia inatumia neno “uasherati” ili kumaanisha matendo fulani ya ngono inje ya ndoa. Mungu anataka waabudu wake ‘wajiepushe na uasherati.’ (1 Wathesalonike 4:3) Uasherati ni kati ya zambi nzito, kama vile uzinifu, uchawi, ulevi, kuabudu sanamu, kuua, na kuiba.​—1 Wakorintho 6:9, 10; Ufunuo 21:8.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO? Sababu moja ni kwamba Biblia inaonya kuwa “Mungu atawahukumu waasherati.” (Waebrania 13:4) Na jambo la maana zaidi, tunapotii sheria za Mungu juu ya mwenendo muzuri kuhusu ngono, tunaonyesha kwamba tunamupenda Yehova Mungu. (1 Yohana 5:3) Pia Mungu anawabariki watu ambao wanashika amri zake.​—Isaya 48:18.

Je, ni vibaya kwa watu ambao hawaoane kuwa na aina yoyote ya uhusiano wa kingono?

‘Uasherati na ukosefu wa usafi wa kila namna ao pupa visitajwe hata kidogo katikati yenu.’​—Waefeso 5:3.

MAMBO AMBAYO WATU WANASEMA Watu wengi wanaamini kwamba hakuna ubaya wowote kwa watu ambao hawaone kuwa na mahusiano ya kingono, kama vile kugusana kwenye viungo vya uzazi, kupeana busu za kukokotana ulimi, na kazalika. Wanasema kwamba kufanya ngono tu ndilo jambo mbaya.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA Inapozungumuzia mazoea mabaya ya kingono, Biblia haitaje tu uasherati lakini inataja pia “unajisi” ao uchafu wa kingono na ‘mwenendo mupotovu.’ (2 Wakorintho 12:21) Ni wazi kwamba kuna aina mbalimbali za uhusiano wa kingono zinazomuchukiza Mungu wakati zinafanywa inje ya ndoa, hata ikiwa watu hawafanye ngono.

Kwa ujumla, kuhusu ngono, Biblia inasema kwamba mwanaume na mwanamuke ambao wameoana ndio tu wanapaswa kuwa na mahusiano ya kingono. Biblia inakataza pia “hamu yenye tamaa ya ngono.” (1 Wathesalonike 4:5) Hilo linamaanisha nini? Fikiria mufano ambao unaweza kutumiwa kuhusu mwanaume ao mwanamuke: Mwanamuke anaweza kuamua kutofanya ngono na muchumba wake. Lakini, anafanya aina fulani ya uhusiano wa kingono pamoja naye. Kwa kufanya hivyo, wanatamani kitu fulani ambacho hakijakuwa chao. Kwa hiyo, wanafanya kosa la “hamu yenye tamaa ya ngono.” Tamaa hiyo ya ngono inakatazwa katika Biblia.​—Waefeso 5:3-5.

Namna gani unaweza kuepuka mwenendo mubaya wa kingono?

“Ukimbieni uasherati.”​—1 Wakorintho 6:18.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO Kulingana na Biblia, watu ambao wanafanya ngono mbele ya kufunga ndoa wanaweza kupoteza urafiki wao pamoja na Mungu.​—Wakolosai 3:5, 6.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA Biblia inawashauria watu ‘waukimbie uasherati.’ (1 Wakorintho 6:18) Hilo linamaanisha kwamba ni lazima mutu aepuke kwa kadiri inavyowezekana kitu chochote ambacho kinaweza kumushawishi ajiingize katika mwenendo mubaya wa kingono. (Methali 22:3) Kwa mufano, ili kuepuka mwenendo mubaya wa kingono, mutu hapaswe kufanya urafiki na watu ambao hawafuate kanuni za Mungu juu ya ngono. Biblia inaonya hivi: “Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima, lakini anayeshirikiana na wajinga atapatwa na mabaya.”​—Methali 13:20.

Kujaza akili mawazo mabaya kunaweza pia kumuongoza mutu awe na mwenendo mubaya wa kingono. (Waroma 8:5, 6) Kwa hiyo, ni jambo la hekima kuepuka miziki, video, vitabu, na kitu chochote ambacho kinaonyesha mambo ya ngono kwa njia isiyofaa ao ambacho kinachochea kwa njia yoyote mwenendo wa kingono ambao unamuchukiza Mungu.​—Zaburi 101:3.