Ya Kwanza kwa Timoteo 5:1-25

  • Namna ya kutendea vijana na wazee (1, 2)

  • Kusaidia wajane (3-16)

    • Kutimiza mahitaji ya watu wa nyumba yako mwenyewe (8)

  • Kuheshimia wazee wenye wanafanya kazi kwa bidii (17-25)

    • ‘Divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako’ (23)

5  Usimukaripie kwa ukali mwanaume mwenye kuzeeka.+ Lakini, umusihi kama baba, na wanaume vijana kama ndugu zako,  na wanamuke wenye kukomaa kama mama, na vijana wanamuke kama dada, kwa mwenendo safi kabisa.  Hangaikia* wajane wenye kuwa wajane kwelikweli.*+  Lakini kama mujane iko* na watoto ao wajukuu, wajifunze kwanza kutenda kwa ushikamanifu kwa Mungu katika nyumba yao wenyewe+ na walipe wazazi wao na wazazi wa wazazi wao kile chenye wanastahili,+ kwa maana hilo linakubaliwa mbele ya macho ya Mungu.+  Sasa mwanamuke mwenye kuwa mujane kwelikweli na mwenye aliachwa bila kitu ameweka tumaini lake kwa Mungu+ na anaendelea kutoa sala za kumulilia Mungu* na kusali usiku na muchana.+  Lakini ule mwenye anajiingiza katika tamaa za mwili amekufa hata kama yeye ni muzima.  Kwa hiyo endelea kutoa maagizo haya,* ili wakuwe bila lawama.  Hakika, kama mutu yeyote hatimize mahitaji ya watu wake mwenyewe, na zaidi sana washiriki wa nyumba yake, amekana imani na ni mubaya kuliko mutu mwenye hana imani.+  Mujane aandikwe kwenye oroza kama haiko chini ya miaka makumi sita (60), kama alikuwa bibi ya bwana mumoja, 10  anajulikana kwa matendo ya muzuri,+ kama alilea watoto,+ kama alikaribisha wageni,+ kama alinawisha miguu ya watakatifu,+ kama alisaidia watu wenye kuteseka,+ na kama alijitolea kwa ajili ya kila kazi ya muzuri. 11  Kwa upande mwingine, usiandike kwenye oroza majina ya wajane wenye wangali vijana, kwa maana wakati tamaa zao za ngono zinakuja kati yao na Kristo, wanataka kuolewa. 12  Na watapata hukumu kwa sababu wameacha wonyesho wao wa kwanza wa imani.* 13  Wakati uleule wanajifunza pia kuwa wavivu, wakizunguka nyumba kwa nyumba; ndiyo, hawakuwe tu wavivu lakini pia wanapiga porojo* na wanajiingiza katika mambo ya watu wengine,+ wakizungumuza juu ya mambo yenye hawapaswe kuzungumuzia. 14  Kwa hiyo, ninapenda wanamuke wajane wenye wangali vijana waolewe,+ wazae watoto,+ wasimamie nyumba, wasimupatie mupinzani nafasi ya kutuchambua-chambua. 15  Kwa kweli, tayari wamoja wao wamegeuzwa pembeni na kumufuata Shetani. 16  Kama mwanamuke yeyote muamini iko* na wajane katika jamaa yake, awasaidie ili kutaniko lisibebe muzigo huo. Halafu kutaniko linaweza kusaidia wale wenye kuwa wajane kwelikweli.*+ 17  Wazee wenye wanasimamia kwa njia ya muzuri+ waonwe kuwa wanastahili heshima mara mbili,+ zaidi sana wale wenye wanafanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.+ 18  Kwa maana andiko linasema: “Haupaswe kufunga kinywa cha ngombe-dume wakati anakanyanga-kanyanga nafaka,”+ pia, “Mufanyakazi anastahili malipo yake.”+ 19  Usikubali shitaka juu ya mwanaume muzee* isipokuwa kwa ushuhuda wa mashahidi wawili ao watatu (3).+ 20  Wale wenye wanazoea kufanya zambi,+ uwakaripie+ mbele ya watazamaji wote, ili ikuwe onyo kwa wengine.* 21  Ninakuagiza kwa uzito mbele ya Mungu na Kristo Yesu na malaika wenye walichaguliwa, kwamba ushike maagizo haya bila upendeleo wala ubaguzi wowote.+ 22  Usiweke mikono yako juu ya mutu yeyote haraka-haraka;*+ na usishiriki katika zambi za watu wengine; endelea kuwa na mwenendo safi. 23  Usiendelee kunywa maji tu,* lakini ukunywe divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako na ugonjwa wako wa mara kwa mara. 24  Zambi za watu fulani zinajulikana mbele ya watu wote, na zinaongoza moja kwa moja kwenye hukumu, lakini zambi za watu wengine zinakuwa wazi kisha wakati fulani.+ 25  Vilevile pia, matendo ya muzuri yanajulikana mbele ya watu wote+ na yale yenye hayajulikane hayawezi kuendelea kufichwa.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Heshimia.”
Ao “wajane wenye kuwa kabisa katika uhitaji”; ni kusema, wenye hawana mutu wa kuwasaidia.
Ao “eko.”
Ao “dua.”
Ao “amri hizi.”
Ao “ahadi yao ya kwanza.”
Porojo ni kusema mubaya juu ya watu na maisha yao.
Ao “eko.”
Ao “wajane wenye kuwa kabisa katika uhitaji”; ni kusema, wenye hawana mutu wa kuwasaidia.
Ao “juu ya muzee.”
Tnn., “ili wengine waogope.”
Ni kusema, usiweke mutu yeyote haraka-haraka kwenye madaraka.
Ao “Acha kunywa maji tu.”