Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mashauri Yanayoweza Kukusaidia Uepuke Kununua-Nunua Vitu Bila Mupango

Mashauri Yanayoweza Kukusaidia Uepuke Kununua-Nunua Vitu Bila Mupango

Matangazo ya biashara yanaweza kutuchochea kununua​-nunua vitu bila mupango, lakini pia tamaa na tabia zetu zinaweza kutuchochea kufanya hivyo. Tuchunguze mashauri sita yanayoweza kukusaidia uepuke kununua​-nunua vitu bila mupango.

  1. Kataa kabisa kununua vitu bila mupango. Je, unafurahia sana kuenda kununua vitu na kubishana-bishana juu ya bei? Ikiwa una tabia hiyo, unaweza kushawishiwa kununua vitu bila mupango. Ili kushinda tabia hiyo, tulia kwanza na ufikiri juu ya matokeo ambayo utapata huko mbele juu ya kitu ambacho unapanga kununua, kuwa nacho nyumbani na pia kukitunza. Fikiria kitu ulichonunua wakati uliopita kwa sababu ya kuchochewa tu na tamaa na kisha ukasikitika baadaye. Chukua wakati wa kufikiri mbele ya kukamata uamuzi wa mwisho.

  2. Epuka kununua vitu ili tu kutuliza hasira yako. Ni kweli kwamba kuenda kununua vitu kunaweza kukutuliza kwa muda. Lakini hasira yako inaporudia tena, unaweza kuchochewa hata zaidi kuenda tena kununua​-nunua vitu ili tu kutuliza hasira yako. Kuliko kuenda kununua vitu ili tu kutuliza hasira yako, ni vizuri kutembelea marafiki wanaoweza kukutegemeza, ao kufanya mazoezi fulani ya mwili, kama vile kutembea kwa miguu.

  3. Epuka kununua vitu ili tu kujifurahisha. Leo, mahali pa kuuzisha vitu pamegeuza shuguli za kununua vitu kuwa njia ya kujifurahisha. Ijapokuwa unaweza kutembelea mahali kama hapo ao kujifurahisha kwa kuangalia vitu mbalimbali kwenye Internete, jua kwamba vitu vingi ambavyo unaona vimetiwa hapo ili kuchochea tamaa yako ya kuvinunua. Nunua kitu ikiwa tu una mupango kabisa wa kukinunua, na usinunue vitu vingine ambavyo haukupangia.

  4. Chagua marafiki wako kwa uangalifu. Namna ya kuishi ya marafiki wako na mazungumuzo yao vinaweza kuchochea sana tamaa yako. Ikiwa unapenda kununua vitu vingi ili uwe kama marafiki wako, hivyo basi chagua marafiki ambao hawazungumuzie sana mambo ya feza ao vitu vya kimwili.

  5. Tumia kwa akili kadi zako za benki. Kadi za mukopo ao kukubaliwa kuchukua vitu kwenye duka fulani ili ulipe baadaye, vinaweza kukufanya ununue vitu bila kufikiria garama. Jikaze kulipa kila mwezi deni zote ulizochukua kwa njia ya kadi. Ni vizuri pia kujua ikiwa utaombwa kulipa faida za juu, ulinganishe mikopo inayotolewa ili kupata mukopo ambao hautaombwa kurudisha faida ya juu zaidi. Uwe mwangalifu kuhusu kadi za mikopo ambazo zinaomba kurudisha faida ya juu sana lakini zinatoa faida ambazo hauhitaji. Kuliko kununua vitu kupitia kadi za mikopo, linda feza zako ili ununue vitu vingi pamoja kwa kulipa feza moja kwa moja.

  6. Jua mapato yako. Ikiwa haufikirie mapato yako, ni vyepesi kutumia feza ovyoovyo. Andika kila mara ao kila siku matumizi yako ya feza, na jua jumla ya feza ulizo nazo. Kila mwezi andika feza unazopanga kutumia ukifikiria mapato yako na garama ulizofanya mwezi uliopita. Linganisha feza ulizotumia mwezi uliopita na zile unazopanga kutumia sasa. Umuombe rafiki yako ambaye unatumainia ili akusaidie kuelewa mambo yanayohusu feza ambayo hauelewe vizuri.