Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna Bibi na Bwana Wanavyoweza Kuepuka Tabia ya Kuacha Kusemezana

Namna Bibi na Bwana Wanavyoweza Kuepuka Tabia ya Kuacha Kusemezana

TATIZO

Namna gani watu ambao walitoa naziri ya kupendana wanaweza kuacha kusemezana kwa muda wa saa nyingi ao hata kwa muda wa siku fulani? Bibi na bwana, kila mumoja anajiambia, ‘Mwishowe, hatupigane tena.’ Lakini, tatizo lingali, na wote wawili hawajakuwa bado na furaha waliokuwa nayo.

SABABU GANI TATIZO HILO LINATOKEA

Kulipiza kisasi. Bibi na bwana wanaacha kusemezana kwa muda fulani kwa kusudi la kulipiza kisasi. Kwa mufano, bwana anaweza kupanga kufanya mambo fulani mwishoni mwa juma bila kumujulisha bibi yake. Bibi anapojua hilo, anakasirika na anamuita bwana yake kuwa mutu asiyejali wengine. Bwana anamuambia kwamba yeye pia ana tabia ya kukasirika haraka. Bibi anaondoka akiwa mwenye kukasirika na anaacha kusemezana na bwana yake. Ni kama vile anasema, “Unaniumiza, na mimi nitakuumiza.”

Kumutawala mwengine kwa werevu. Bibi na bwana wanaacha kusemezana kwa muda fulani ili kumufanya mwengine akubali maoni yake. Kwa mufano, wazia bibi na bwana wanapanga kusafiri na bibi anataka waende pamoja na wazazi wake pia. Bwana anakataa na kusema: “Nilikuoa wewe, sikuwaoa wazazi wako.” Kisha anaacha kuzungumuza na bibi yake mupaka wakati atakubaliana naye kwamba hawatasafiri pamoja na wazazi wake.

Wakati fulani, unapoona kwamba umekasirika, ni vizuri uache kubishana na bibi ao bwana yako na kungoja utulie kwanza. Kubaki kimya kunaweza kuwa na matokeo mazuri. Biblia inasema kwamba kuna “wakati wa kukaa kimya.” (Mhubiri 3:7) Lakini ikiwa bibi ao bwana anamunyamazia mwenzake kwa kusudi la kulipiza kisasi ao kutumia werevu ili kumukaza mwenzake akubali maoni yake, hilo linafanya ugomvi uendelee na pia linapunguza heshima ambayo wanapaswa kuonyeshana. Munaweza kufanya nini ili jambo hilo lisitokee kati yenu?

MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Jambo la kwanza la kufanya ili kuepuka tabia ya kuacha kusemezana ni kujua kwamba kufanya hivyo hakumalize kabisa tatizo lenu. Ni kweli kwamba kuacha kusemezana na bibi ao bwana yako kwa muda fulani inaweza kuwa njia ya kulipiza kisasi ao njia ya kumulazimisha mwenzako akubali maoni yako. Lakini je, ungependa kumutendea hivyo mutu ambaye ulitoa naziri ya kumupenda? Kuna njia zingine zilizo nzuri zaidi za kumaliza ugomvi.

Uwe na utambuzi. Biblia inasema kwamba upendo “hauchokozeki.” (1 Wakorintho 13:4, 5) Wakati bibi ao bwana yako anasema akiwa mwenye kukasirika maneno kama vile “wewe haunisikilize hata kidogo” ao “sikuzote unafika nyumbani usiku,” usimujibie haraka. Kuliko kukasirika, tafuta kuelewa alitaka kusema nini. Kwa mufano, maneno “wewe haunisikilize hata kidogo” yanaweza kumaanisha “naona kwamba wewe hauchukue maoni yangu kwa uzito.”​—Kanuni ya Biblia: Methali 14:29.

Kumbuka kwamba bibi ao bwana yako ni rafiki yako, wala si adui yako

Punguza sauti yako. Kadiri munavyoendelea kubishana ndivyo mabishano yanavyochacha. Lakini kuna jambo ambalo munaweza kufanya ili mabishano yasichache. Jambo gani? Kitabu kimoja (Fighting for Your Marriage) kinasema hivi: “Kushusha sauti na kukubali maoni ya mwenzako ni njia nzuri unayoweza kutumia ili kupunguza hasira na kumaliza mabishano. Mara nyingi inaomba tu kufanya hivyo ili kumaliza ugomvi.”​—Kanuni ya Biblia: Methali 26:20.

Usijifikirie mwenyewe tu, fikiria pia mwenzako. Biblia inasema hivi: ‘kila mumoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali ile ya yule mutu mwingine.’ (1 Wakorintho 10:24) Ukikumbuka kwamba bibi ao bwana yako ni rafiki yako, wala si adui yako, hautakasirika haraka, hautabishana naye, na hautaacha kusemezana naye kwa muda fulani.​—Kanuni ya Biblia: Mhubiri 7:9.

Kuacha kusemezana na bibi ao bwana yako hakupatane na shauri hili la Biblia: ‘Kila mutu mumoja-mumoja kati yenu na amupende hivyo muke wake kama vile anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwengine, muke anapaswa kumuheshimu sana mume wake.’ (Waefeso 5:33) Unaweza kufanya mapatano wewe na bibi yako ao na bwana yako kwamba katika ndoa yenu hamutaacha kusemezana hata siku moja.

[Caption on page 4]

Tafuta habari zaidi za kusaidia familia kwenye adresi yetu ya Internete www.dan124.com