Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Ulimwengu

Habari Fulani za Ulimwengu

Arktiki

Peter Wadhams, mwalimu wa fizikia ao elimu ya mambo ya bahari kwenye Masomo ya Juu ya Cambridge, huko Uingereza, anasema hivi: “Kiasi cha barafu katika majira ya joto ni sehemu moja ya ine tu ya barafu iliyokuwa miaka 30 iliyopita.” Katika mwaka wa 2012, mashua 50 hivi zilitumia Njia ya Bahari ya Kaskazini ambayo ilifunguliwa kwa sababu ya kuongezeka kwa joto duniani.

Ulimwengu

Imegunduliwa kwamba maziwa ya matiti ya akina mama katika siku zinazofuata kuzaliwa kwa mutoto yana zaidi ya aina 700 ya bakteria, ni kusema, bakteria nyingi zaidi kuliko zile ambazo wachunguzi walitazamia. Wachunguzi wangali wanafanya uchunguzi ili kujua faida za kazi ya bakteria hizo katika mufumo wa kusaga chakula na mufumo wa kulinda mwili wa mutoto muchanga.

Uingereza

Katika uchunguzi ambao wanasayansi wa inchi ya Uingereza walifanya juu kuendesha motokari, ilionekana kwamba waendeshaji wa motokari wanaosumbuliwa na mafua walikuwa wenye kutenda polepole sana kuliko waendeshaji wa motokari walevi.

Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Katika Afrika, mauaji ya makumi ya maelfu ya tembo yanafanywa kila mwaka ili kupata pembe za tembo. Watu wengine wanaita mauaji hayo kuwa “mauaji ambayo hayajapata kufanywa.” Wakati fulani, tembo wengi walipigwa risasi kwenye vichwa, labda na watu ambao walikuwa ndani ya ndege ya helikopta.

Australia

Katika miaka 27 iliyopita, miamba mikubwa ya chini ya bahari imepoteza nusu ya matumbawe yake ao majiwe laini ya baharini yanayotokana na mukusanyo wa wanyama wadogo wa baharini. Wanasayansi wanasema kwamba uharibifu huo unatokana na zoruba za kitropiki, kuongezeka kwa viumbe wa baharini wanaoitwa pweza [Acanthaster planci], na kupoteza rangi kwa matumbawe ambako kunatokana na joto kali zaidi la bahari.