Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maoni Ya Biblia

Yesu

Yesu

Yesu Ni Mungu?

‘Hakuna mwanadamu ambaye amemuona Mungu wakati wowote.’​—Yohana 1:18.

MAMBO WATU WANASEMA

: Watu wengi wanaamini kuwa Yesu si Mungu. Lakini, wengine wanaonyesha maandiko ya Biblia ambayo wanawazia yanasema kuwa Yesu ni sawa na Mungu.

MAMBO BIBLIA INASEMA

: Biblia haiseme kuwa Yesu ndiye Mungu Mweza-Yote ao kwamba yeye ni sawa na Mungu. Lakini, inafundisha waziwazi kama Mungu ni mukubwa kuliko Yesu. Kwa mufano, Biblia inataja maneno haya ambayo Yesu mwenyewe alisema: ‘Baba ni mukubwa kuliko mimi.’ (Yohana 14:28) Biblia inasema tena hivi: ‘Hakuna mwanadamu ambaye amemuona Mungu wakati wowote.’ (Yohana 1:18) Yesu hawezi kuwa Mungu kwa sababu watu wengi walimuona.

Wafuasi wa kwanza wa Yesu hawakusema kuwa Yesu ni Mungu. Kwa mufano, Yohana muandikaji wa injili alisema hivi juu ya mambo aliyoandika: ‘Haya yameandikwa ili mupate kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu.’​—Yohana 20:31. *

Yesu alizaliwa wakati gani?

‘Kulikuwa wachungaji wakiishi inje, wakichunga makundi yao usiku.’​—Luka 2:8.

MAMBO WATU WANASEMA

: Watu fulani wanafanya sikukuu ya Noeli tarehe 25 Mwezi wa 12, tarehe wanayowazia kuwa ndiyo siku ya kuzaliwa kwa Yesu. Wengine wanafanya sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu mwanzo-mwanzo wa Mwezi wa 1.

MAMBO BIBLIA INASEMA

: Biblia haionyeshe tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu. Lakini, inasema kuwa wakati Yesu alizaliwa, ‘kulikuwa wachungaji wakiishi inje, wakichunga makundi yao usiku.’ (Luka 2:8) Haingewezekana wachungaji hao wachunge makundi yao inje usiku katika Mwezi wa 12 na Mwezi wa 1. Sababu gani?

Katika eneo ambamo Yesu alizaliwa kuna baridi kali Mwezi wa 12 na Mwezi wa 1. Kuhusu wakati huo wa mwaka, Biblia inasema kwamba watu walikuwa “wakitetemeka . . . kwa sababu ya manyunyu ya mvua” na ‘haikuwezekana kusimama inje.’ (Ezra 10:9, 13; Yeremia 36:22) Huo haukuwa wakati wa mwaka ambao wachungaji ‘wangeishi inje’ pamoja na makundi yao.

Yesu alifufuka kabisa kisha kufa kwake?

‘Mungu alimufufua Yesu kutoka kwa wafu.’​—Matendo 3:15.

MAMBO WATU WANASEMA

: Watu fulani wanafikiri kuwa haiwezekane mutu yeyote, hata na Yesu pia, afufuliwe kisha kufa.

MAMBO BIBLIA INASEMA

: Yesu aliwafundisha wafuasi wake kwamba ‘angepatwa na mambo mengi . . . na kuuawa, na siku ya tatu afufuliwe.’ (Mathayo 16:21) Biblia inasema kuwa kisha kuuawa kwake na kufufuliwa, Yesu alitokea watu zaidi ya 500. (1 Wakorintho 15:6) Watu hao waliomuona hawakuwa na shaka lolote kwamba alifufuliwa kutoka kwa wafu. Walikuwa hata tayari kufa kwa sababu ya kuamini jambo hilo!​—Matendo 7:51-60; 12:1, 2.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Biblia inafundisha kwamba kifo cha Yesu na ufufuo wake vilifungulia wanadamu njia ya kuishi katika dunia Paradiso ambayo Biblia inaahidi. (Zaburi 37:11, 29; Ufunuo 21:3, 4) Kwa sababu ya upendo ambao Yesu na Baba yake Yehova, Mungu Mweza​-Yote, walituonyesha, tuna tumaini la kuishi kwa furaha na bila kufa katika dunia hii itakayokuwa Paradiso.​—Yohana 3:16; Waroma 6:23.

^ Biblia haifundishe kama Mungu ana bibi kwelikweli ambaye alizaa naye watoto. Lakini, inamuita Yesu “Mwana wa Mungu” kwa sababu Yesu aliumbwa moja kwa moja na Mungu, akiwa na sifa ao tabia zinazofanana na za Baba yake.