Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Bawa la Kipepeo Linalofyonza Mwangaza

Bawa la Kipepeo Linalofyonza Mwangaza

ILI KUPUNGUZA matumizi ya makaa ya mawe, gesi, petroli, wanasayansi wanafanya nguvu yao yote ili vifaa vya kukusanya mwangaza wa jua vifanye kazi vizuri. Mwanasayansi mumoja alisema hivi: “Suluhisho kwa tatizo hili . . . linaweza kuwa liko mbele ya macho yetu.”

Magamba kwenye bawa la kipepeo yana mashimo yanayofanana na sega la asali

Fikiria jambo hili: Ili miili yao iendelee kuwa na joto wakati wa baridi, vipepeo vinapanua mabawa yao kwenye jua. Mabawa ya aina fulani ya vipepeo vinavyoitwa ­swallowtail ina uwezo muzuri wa kukamata na kufyonza mwangaza wa jua. Jambo linalowezesha kipepeo kufyonza mwangaza ni chembe inayofanya mabawa yake kuwa meusi na namna magamba yake madogo-madogo yanayofunika mabawa yanavyoingiana. Magamba hayo yana mashimo mengi yenye kufanana na yale ya sega la asali na ambayo inatenganishwa na mistari yenye kuwa na sura ya herufi V iliyogeuzwa ambayo inaingiza mwangaza katika mashimo hayo. Magamba yenye kuingiana yanayofunika mabawa ya kipepeo yanapokea mwangaza huo, na kufanya mabawa yake kuwa meusi sana na hilo linafanya mwili wa kipepeo upate joto nyingi.

Gazeti moja linasema hivi: “Mabawa ya kipepeo ni kati ya vitu vilivyo teketeke sana, lakini vimewatolea wachunguzi mawazo mazuri mengi ili kutengeneza vifaa vipya vinavyotoa gesi ya hidrojeni mara mbili, ambayo ni nishati ao nguvu itakayotumiwa wakati ujao na inayotoka katika maji na mwangaza wa jua.” (Science Daily) Wachunguzi watatumia mawazo hayo pia kutengeneza vifaa vya kusaidia kuona mbali na vifaa vinavyosaidia kunasa mwangaza wa jua.

Unawaza nini? Uwezo wa bawa la kipepeo wa kufyonza mwangaza wa jua ulitokana na mageuzi ao uliumbwa?