Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Namna ya Kukataa Ombi la Mutoto

Namna ya Kukataa Ombi la Mutoto

TATIZO

Hata kama unakataa ombi la mutoto, yeye hatatosheka. Kila mara unapomuambia hapana, namna yake * ya kuitikia inatia uvumulivu wako katika jaribu. Jambo lolote unalosema na unalofanya haliwezi kumutuliza, na mwishowe unaona kwamba hakuna jambo lingine la kufanya, basi unalazimika kujibu ombi lake. Mara ingine tena, ijapokuwa ulikuwa umekataa kabisa, unalazimika kuitika bila kutaka.

Unaweza kujifunza namna ya kutokubali kila ombi la mutoto. Tufikirie kwanza mambo fulani unayopaswa kujua kuhusu kukataa ombi la mutoto.

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Kukataa ombi la mutoto hakumaanishe kama uko mukali. Wazazi fulani hawakubaliane na wazo hilo, wanasema kwamba ni vizuri kufikiri na mutoto, kumuelezea sababu gani unakataa jambo analosema, ao hata kujaribu kupatana naye. Lakini, wanasema ni vizuri kuepuka kukataa ombi la mutoto, ili asihuzunike.

Kwa kweli, mwanzoni “kukataa” kunaweza kumuvunja mutoto moyo. Lakini kufanya hivyo kunamufundisha jambo la maana, anaelewa kwamba katika maisha ya kila siku kuna mipaka ambayo watu hawapaswe kuvuka. Kwa upande mwengine, unapokubali kila jambo mutoto anasema unapunguza mamlaka yako na unamufanya mutoto wako afikiri kwamba anaweza kukulazimisha kufanya jambo fulani kwa kulia-lia kila wakati anataka kitu fulani. Ukiendelea kukataa kila kitu anachoomba, atakukasirikia. Lakini, je, mutoto anaweza kumuheshimia kabisa muzazi anayekubali kwa urahisi kila kitu anachoombwa?

Kukataa ombi la mutoto kunamutayarisha kwa ajili ya miaka ya ujana na ya ukubwa. Kunamusaidia ajue faida ya kujinyima mambo fulani. Mutoto anayejua jambo hilo la maana hatakubali kwa urahisi kuchochewa na vijana wengine ili kutumia dawa za kulewesha ao kufanya uasherati mbele ya kufanya ndoa.

Pia, kumuambia mutoto hapana kunamutayarisha kwa ajili ya miaka ya ukubwa. David Walsh anaandika hivi: “Ukweli ni kwamba, sisi [watu wazima] hatupate sikuzote mambo tunayohitaji. Hatuwasaidie watoto wetu hata kidogo wakati tunawapatia kila kitu ambacho wanaomba.” *

 MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Fuatia muradi wako. Unataka mutoto wako akomae, awe na uwezo wa kuzuia tamaa zake, na apate matokeo mazuri wakati atakuwa mutu muzima. Lakini hautafikia muradi huo ikiwa unamupatia kila kitu ambacho anaomba. Biblia inasema kwamba ikiwa mutu fulani ‘anabembelezwa tangu ujana wake, baadaye atakuwa mutu asiye na shukrani.’ (Methali 29:21) Kwa hiyo, kumuambia hapana, ni njia ya kumuzoeza mutoto muzuri. Mazoezi hayo yatamusaidia mutoto wako, hayatamuumiza.—Kanuni ya Biblia: Methali19:18.

Ikiwa umekataa ombi lake, usibadilike. Mutoto wako yuko chini ya mamlaka yako. Kwa hiyo, wakati umemuambia hapana, si lazima kubishana naye kama kwamba ana mamlaka ya kukuamulia. Bila shaka, watoto wanapoendelea kukomaa, ni lazima wawe na ‘nguvu za ufahamu ambazo zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.’ (Waebrania 5:14) Kwa hiyo, si mubaya kufikiri na mutoto. Hata hivyo, usijiingize katika mabishano yasiyo na mwisho na mutoto wako ili kumuelezea sababu gani unasema hapana. Kama unaendelea kubishana na mutoto wako, ataona kwamba kukataa kwako ni pendekezo tu, si uamuzi.—Kanuni ya Biblia: Waefeso 6:1.

Shikamana na uamuzi wako. Mutoto wako anaweza kutia uamuzi wako katika jaribu ikiwa analia-lia ao anaendelea kukuomba ili utimize ombi lake. Ikiwa hilo linatokea, unaweza kufanya nini? Kitabu kimoja kinatoa shauri hili: “Usiendelee kuwa pamoja naye. Umuambie hivi: ‘Kama unakasikika, sawa, lakini sitaki tena kukusikiliza. Enda katika chumba chako. Ulilie huko mupaka utanyamaza.” (Loving Without Spoiling) Mwanzoni, inaweza kuwa vigumu kwako kumuambia hivi, na mutoto anaweza kuwa pia na magumu ya kukubali. Lakini, wakati ataona kwamba unashikamana na uamuzi wako, basi, ataanza kuregea.—Kanuni ya Biblia: Yakobo 5:12.

Usiseme hapana ili tu kuonyesha mamlaka yako kama muzazi

Uwe na usawaziko. Usimuambie mutoto hapana ili tu kutafuta kumuonyesha kwamba wewe ni muzazi. Lakini, “usawaziko wenu na ujulikane.” (Wafilipi 4:5) Kuna nyakati ambazo unaweza kukubali ombi la mutoto wako, lakini usikubali kwa sababu ya kulia-lia kwake, ukubali kwa sababu anaomba kitu anachohitaji kabisa.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:21.

^ fu. 4 Kanuni zinazozungumuziwa katika habari hii zinahusu vijana wa kiume na wa kike.

^ fu. 10 Yanatoka katika kitabu No: Why Kids—of All Ages—Need to Hear It and Ways Parents Can Say It.