Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 36

Armagedoni Ni Habari Njema!

Armagedoni Ni Habari Njema!

“Yakawakusanya pamoja . . . kwenye . . . Armagedoni.”​—UFU. 16:16.

WIMBO 150 Mtafute Mungu Upate Ukombozi

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. (a) Juu ya nini Armagedoni ni habari njema kwa familia ya wanadamu? (b) Tutazungumuzia maulizo gani katika habari hii?

WATU fulani wanasema kama “Armagedoni” ni vita ya mabombe ya nyukilia ao uharibifu wa mazingira. Lakini, mambo yenye Biblia inasema juu ya Armagedoni ni habari njema na ni yenye kufurahisha! (Ufu. 1:3) Vita ya Armagedoni haitaharibu wanadamu wote lakini itaokoa familia ya wanadamu! Namna gani?

2 Biblia inaonyesha kama vita ya Armagedoni itaokoa familia ya wanadamu kwa kumaliza utawala wa wanadamu. Vita hiyo itaokoa familia ya wanadamu kwa kuharibu watu waovu na kulinda watu wenye haki. Pia, itaokoa familia ya wanadamu kwa kulinda dunia yetu isiharibiwe. (Ufu. 11:18) Ili kutusaidia kuelewa muzuri ile mambo, tuzungumuzie basi maulizo ine yenye kufuata: Armagedoni ni nini? Kutakuwa matukio gani mbele ya Armagedoni? Tunaweza kufanya nini ili tukuwe kati ya watu wenye wataokoka Armagedoni? Tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuwa waaminifu kadiri Armagedoni inakaribia?

ARMAGEDONI NI NINI?

3. (a) Neno “Armagedoni” maana yake nini? (b) Kulingana na Ufunuo 16:14, 16, juu ya nini tunasema kama Armagedoni haiko nafasi fulani ya kwelikweli ku dunia?

3 Soma Ufunuo 16:14, 16. Neno “Armagedoni” linapatikana mara moja tu mu Maandiko, na linatokana na neno la Kiebrania lenye kumaanisha “Mulima wa Megido.” (Ufu. 16:16; maelezo ya chini) Megido ulikuwa muji mumoja wenye ulikuwa katika Israeli ya zamani. (Yos. 17:11) Lakini Armagedoni haiko jina la nafasi yoyote ya kwelikweli ku dunia. Kwa kweli, ni hali ambamo “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” wanakusanywa ili kumupinga Yehova. (Ufu. 16:14) Lakini, mu habari hii, tutatumia pia neno “Armagedoni” ili kumaanisha vita yenye itatokea mara moja kisha kukusanywa kwa wafalme wa dunia. Ni nini inaonyesha kama Armagedoni ni nafasi ya mufano? Jambo la kwanza, hakuna mulima wa kwelikweli wenye kuitwa Megido. Jambo la pili, eneo lenye kuzunguka muji wa Megido ni la kidogo sana, “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” na majeshi yao na silaha zao hawawezi kuenea pale. Jambo la tatu, kama vile tutaona katika habari hii, vita ya Armagedoni itaanza wakati “wafalme” wa dunia watashambulia watu wa Mungu, wenye kuishi nafasi mbalimbali mu dunia.

4. Juu ya nini Mungu alihusianisha vita yake kubwa ya mwisho na Megido?

4 Juu ya nini Yehova alihusianisha vita yake kubwa ya mwisho na Megido? Zamani, vita za mingi zilipiganwa mu muji wa Megido na mu Bonde la Yezreeli lenye lilikuwa karibu. Wakati fulani, Yehova alisaidia watu wake ili washinde vita hizo. Kwa mufano, “pembeni ya maji ya Megido,” Mungu alimusaidia Baraka, Muamuzi wa Israeli, ashinde jeshi la Wakanaani lenye liliongozwa na mukubwa wa jeshi mwenye aliitwa Sisera. Baraka na Debora, nabii mwanamuke, walimushukuru Yehova juu ya ushindi wenye walipata kwa njia ya muujiza. Waliimba hivi: “Nyota zilipigana zikiwa mbinguni . . . zilipigana na Sisera. Maji mengi ya Kishoni yaliwafagilia mbali.”​—Amu. 5:19-21.

5. Kuko tofauti gani kubwa kati ya vita ya Armagedoni na vita yenye Baraka alipigana?

5 Baraka na Debora walimalizia wimbo wao kwa kusema hivi: “Na maadui wako wote waangamie vile, Ee Yehova, lakini wenye kukupenda wangae kama jua wakati linatokea katika utukufu wake.” (Amu. 5:31) Vilevile, ku vita ya Armagedoni, maadui wa Mungu wataharibiwa, lakini watu wenye kumupenda Mungu wataokolewa. Hata hivyo, kuko tofauti moja kubwa kati ya vita ya Armagedoni na vita yenye Baraka alipigana. Ku vita ya Armagedoni, watu wa Mungu hawatapigana. Hawatakuwa hata na silaha! ‘Watakuwa na nguvu kama wanaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini’ katika Yehova na katika majeshi yake ya mbinguni.​—Isa. 30:15; Ufu. 19:11-15.

6. Yehova anaweza kutumia njia gani ili kuharibu maadui wake ku vita ya Armagedoni?

6 Mungu atatumia njia gani ili kuharibu maadui wake ku vita ya Armagedoni? Anaweza kutumia njia za mingi. Kwa mufano, anaweza kutumia matetemeko ya inchi, mvua ya majiwe, na umeme wa radi. (Yob. 38:22, 23; Eze. 38:19-22) Anaweza kufanya maadui wake wauane. (2 Ny. 20:17, 22, 23) Na anaweza kutumia malaika wake ili waue watu waovu. (Isa. 37:36) Hata Mungu atumie njia gani, atapata ushindi kabisa. Maadui wake wote wataharibiwa. Na watu wote wenye haki wataokolewa.​—Mez. 3:25, 26.

KUTAKUWA MATUKIO GANI MBELE YA ARMAGEDONI?

7-8. (a) Kulingana na 1 Watesalonike 5:1-6, ni tangazo gani lenye haliko la kawaida lenye viongozi wa ulimwengu watafanya? (b) Juu ya nini tangazo hilo litakuwa uongo hatari?

7 Tangazo la “amani na usalama” litafanywa mbele ya “siku ya Yehova.” (Soma 1 Watesalonike 5:1-6.) Mu 1 Watesalonike 5:2, “siku ya Yehova” maana yake ni “ile taabu kubwa.” (Ufu. 7:14) Ni nini itatuonyesha kama ile taabu kubwa inataka kuanza? Biblia inasema kama kutakuwa tangazo fulani lenye haliko la kawaida kabisa. Tangazo hilo litakuwa alama yenye itaonyesha kama taabu kubwa inataka kuanza.

8 Tangazo hilo njo tangazo lenye lilitabiriwa la “amani na usalama.” Juu ya nini viongozi wa serikali watatangaza vile? Je, viongozi wa dini watajiunga nao? Pengine. Hata hivyo, tangazo hilo litakuwa tu uongo mwingine wenye utatoka kwa pepo wachafu. Lakini, uongo huo utakuwa hatari zaidi juu utafanya watu wawaze kama kuko usalama, kumbe taabu kubwa zaidi inataka kuanza. Kwa kweli, “uharibifu wa kushitukia utakuja juu yao mara moja, kama vile maumivu ya kuzaa ya mwanamuke mwenye mimba.” Halafu watumishi washikamanifu wa Yehova? Pengine watashangaa wakati siku ya Yehova itaanza kwa kushitukia, lakini watakuwa tayari kwa ajili ya siku hiyo.

9. Je, Yehova ataharibu ulimwengu wote wa Shetani mara moja? Fasiria.

9 Yehova hataharibu ulimwengu wote wa Shetani mara moja, kama vile alifanya wakati wa Noa. Lakini, ataharibu sehemu moja kwanza, na kisha ataharibu sehemu zingine. Kwanza, ataharibu Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo. Kisha, ku Armagedoni, ataharibu sehemu zingine zenye kubakia za ulimwengu wa Shetani, ni kusema, mupangilio wa politike, wa kijeshi, na wa biashara. Tuzungumuzie basi ile matukio mbili makubwa.

10. Kulingana na Ufunuo 17:1, 6 na 18:24, juu ya nini Yehova ataharibu Babiloni Mukubwa?

10 “Hukumu juu ya ule kahaba mukubwa.” (Soma Ufunuo 17:1, 6; 18:24.) Babiloni Mukubwa amechafua sana jina la Mungu. Amefundisha mambo ya uongo juu ya Mungu. Amefanya ukahaba wa kiroho kwa kufanya mapatano na watawala wa dunia. Ametesa watu wake na kuwachukua feza zao. Na amemwanga damu ya mingi, hata damu ya watumishi wa Mungu. (Ufu. 19:2) Namna gani Yehova ataharibu Babiloni Mukubwa?

11. “Munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa” ni nani, na namna gani Mungu atamutumia ili kuharibu Babiloni Mukubwa?

11 Yehova atatumia “pembe kumi (10)” za ule “munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa” ili kuharibu “ule kahaba mukubwa.” Ule munyama wa pori wa mufano anafananisha Umoja wa Mataifa. Zile pembe kumi zinafananisha serikali za ulimwengu za leo zenye zinaunga mukono Umoja wa Mataifa. Kwa wakati wenye Mungu ameweka, serikali hizo zitamugeukia Babiloni wa mufano. ‘Zitamuacha bila kitu na uchi,’ kwa kumunyanganya mali zake na kwa kuonyesha waziwazi uovu wake. (Ufu. 17:3, 16) Uharibifu huo wa haraka, wenye utafanyika kama vile mu siku moja, utashangaza sana wale wenye walimuunga mukono. Watashangaa sana kwa sababu amejivuna siku mingi kwa kusema hivi: “Ninakaa nikiwa malkia, mimi siko mujane, na sitaona maombolezo hata kidogo.”​—Ufu. 18:7, 8.

12. Yehova hataruhusu mataifa ifanye nini, na juu ya nini?

12 Mungu hataruhusu mataifa iharibu watu wake. Wanajivunia kuitwa kwa jina lake, na wametii amri yake yenye inaomba watu watoke mu Babiloni Mukubwa. (Mdo. 15:16, 17; Ufu. 18:4) Pia, wametumika sana ili kusaidia watu wengine watoke mu Babiloni Mukubwa. Kwa hiyo, watumishi wa Yehova ‘hawatapokea sehemu ya mapigo [ya Babiloni Mukubwa].’ Lakini, imani yao itajaribiwa.

Kila nafasi kwenye watu wa Mungu watapatikana ku dunia, watamutumainia wakati watashambuliwa (Picha hii inapatana na fungu la 13) *

13. (a) Gogu ni nani? (b) Kulingana na Ezekieli 38:2, 8, 9, ni nini itafanya Gogu ashambulie watu wa Mungu?

13 Shambulizi la Gogu. (Soma Ezekieli 38:2, 8, 9.) Kisha dini zote za uongo kuharibiwa, watu wa Mungu watakuwa kama vile muti moja tu wenye unabakia kisha upepo mukali kupita. Kwa kweli, Shetani atakasirika sana. Ataonyesha kasirani yake kwa kutumia ‘maneno machafu yenye kuongozwa na roho wachafu,’ ni kusema, habari za uongo kutoka kwa pepo wachafu, ili kuchochea muungano wa mataifa ushambulie watumishi wa Yehova. (Ufu. 16:13, 14) Muungano huo unaitwa “Gogu wa inchi ya Magogu.” Wakati mataifa itashambulia watu wa Yehova, vita ya Armagedoni itaanza.​—Ufu. 16:16.

14. Gogu atafikia kutambua nini?

14 Gogu atatumainia “mukono [wake] wa nyama,” ni kusema, majeshi yake yenye nguvu. (2 Ny. 32:8) Sisi, tutamutumainia Yehova Mungu wetu; lakini mataifa itaona jambo hilo kuwa upumbavu. Juu ya nini? Juu Babiloni Mukubwa alikuwa na nguvu, lakini miungu yake haikumuokoa ili asiharibiwe na “munyama wa pori” na “pembe [zake] kumi”! (Ufu. 17:16) Kwa hiyo, Gogu atawaza kama atatuharibu kwa vyepesi. Atashambulia watu wa Yehova “kama mawingu yenye kufunika inchi.” (Eze. 38:16) Lakini, bila kukawia, Gogu atatambua kama ameingia mu mutego. Kama vile Farao na majeshi yake walitambua kama walikuwa wanapigana na Yehova ku Bahari Nyekundu, Gogu naye atafikia kutambua kama iko anapigana na Yehova.​—Kut. 14:1-4; Eze. 38:3, 4, 18, 21-23.

15. Yesu atafanya nini ku vita ya Armagedoni?

15 Kristo na majeshi yake ya mbinguni watapigania watu wa Mungu na kuharibu majeshi ya Gogu. (Ufu. 19:11, 14, 15) Lakini, ni nini itamupata Shetani, adui mukubwa wa Yehova, mwenye alidanganya mataifa na kuichochea ishambulie watu wa Mungu ku vita ya Armagedoni? Yesu atamutupa yeye na pepo wake wachafu mu abiso, kwenye watafungwa kwa miaka elfu moja.​—Ufu. 20:1-3.

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI TUOKOKE VITA YA ARMAGEDONI?

16. (a) Namna gani tunaonyesha kama ‘tunamujua Mungu’? (b) Juu ya nini kumujua Mungu kutatuletea baraka ku Armagedoni?

16 Ikuwe tuko wapya ao wa zamani katika kweli, ili tuokoke vita ya Armagedoni, tunapaswa kuonyesha kama ‘tunamujua Mungu’ na kama ‘tunatii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.’ (2 Te. 1:7-9) Tunaonyesha kama ‘tunamujua Mungu’ wakati tunajua mambo yenye anapenda, mambo yenye anachukia, na kanuni zake. Pia, tunaonyesha kama tunamujua Mungu wakati tunamupenda na kumutii na kushikamana na yeye tu. (1 Yo. 2:3-5; 5:3) Wakati tunaonyesha kama tunamujua Mungu, tunapata pendeleo la ‘kujulikana naye,’ na hilo litafanya tuokoke vita ya Armagedoni! (1 Ko. 8:3) Sababu gani? Kwa sababu ‘kujulikana naye’ maana yake kukubaliwa naye.

17. ‘Kutii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu,’ maana yake nini?

17 “Habari njema juu ya Bwana wetu Yesu” inatia ndani kweli zote zenye Yesu alifundisha, zenye zinapatikana mu Neno la Mungu. Tunatii habari njema wakati tunaitumia mu maisha yetu. Tunafanya vile wakati tunatia Ufalme pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu, wakati tunafuata kanuni za Mungu za haki, na kuhubiria wengine juu ya Ufalme wa Mungu. (Mt. 6:33; 24:14) Pia, tunafanya vile wakati tunategemeza ndugu za Kristo watiwa-mafuta wakati wanatimiza madaraka yao mazito.​—Mt. 25:31-40.

18. Namna gani watumishi wa Mungu watiwa-mafuta watarudishia “kondoo wengine” mema yenye waliwatendeaka?

18 Hivi karibuni, watumishi wa Mungu watiwa-mafuta watarudishia “kondoo wengine” mema yenye waliwatendeaka. (Yoh. 10:16) Namna gani? Mbele vita ya Armagedoni ianze, wale 144 000 watakuwa wameenda mbinguni na kuwa viumbe wa roho wenye hawawezi kufa. Kwa hiyo, watakuwa kati ya majeshi ya mbinguni yenye itamuponda Gogu na kulinda “kundi kubwa la watu,” wenye kufananishwa na kondoo. (Ufu. 2:26, 27; 7:9, 10) Kwa kweli, kundi kubwa la watu watafurahi sana kwa sababu walitegemeza watumishi wa Yehova watiwa-mafuta wakati walikuwa wangali ku dunia!

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI TUENDELEE KUWA WAAMINIFU KADIRI MWISHO UNAKARIBIA?

19-20. Hata tukuwe na magumu gani, tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuwa waaminifu kadiri Armagedoni inakaribia?

19 Mu siku hizi za mwisho zenye kuwa nguvu kuvumilia, watumishi wengi wa Yehova wako wanapata magumu. Lakini, tunaweza kuvumilia kwa furaha. (Yak. 1:2-4) Jambo moja lenye linaweza kutusaidia sana ni kuendelea kusali kwa moyo wote. (Lu. 21:36) Pia, tunapaswa kutenda kulingana na sala zetu kwa kujifunza Neno la Mungu kila siku na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunajifunza, na pia juu ya unabii wenye kushangaza wenye unazungumuzia mambo yenye itatokea mu siku zetu. (Zb. 77:12) Kama tunafanya ile mambo, na kuhubiri habari njema kwa bidii, imani yetu itakuwa yenye nguvu na tutaendelea kuwa na tumaini!

20 Wazia namna utafurahi sana wakati Babiloni Mukubwa atakuwa ameharibiwa na wakati vita ya Armagedoni itakuwa imeisha! Jambo la maana zaidi, wazia namna utakuwa mwenye furaha kabisa wakati kila mutu ataheshimia jina la Mungu na haki yake ya kutawala! (Eze. 38:23) Kwa kweli, Armagedoni ni habari njema kwa watu wenye kumujua Mungu, wenye kumutii Mwana wake, na kuvumilia mupaka mwisho.​—Mt. 24:13.

WIMBO 143 Endeleeni Kufanya Kazi, Kesheni, na Kusubiri

^ fu. 5 Watu wa Yehova wamengojea Armagedoni kwa wakati murefu. Katika habari hii, tutazungumuzia Armagedoni ni nini, kutakuwa matukio gani mbele ya Armagedoni, na mambo yenye tunaweza kufanya ili tuendelee kuwa waaminifu kadiri mwisho unakaribia.

^ fu. 71 MAFASIRIO YA PICHA: Mambo ya kuogopesha itatokea karibu na sisi. Wakati huo, (1) tutahubiri kwa bidii kadiri inawezekana, (2) tutaendelea kuwa na programu yetu ya kujifunza, na (3) tutaendelea kutegemea Mungu ili kupata ulinzi.

^ fu. 85 MAFASIRIO YA PICHA: Polisi wanatafuta kuingia kwa nguvu mu nyumba ya familia fulani ya Kikristo, yenye inatumaini kama Yesu na malaika wake wanaona mambo yenye iko inatendeka.