Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Magonjwa ya Akili Ni Tatizo Yenye Kuenea mu Dunia Yote

Magonjwa ya Akili Ni Tatizo Yenye Kuenea mu Dunia Yote

“Kila mara nakuwaka na mahangaiko ya akili, hata bila sababu.”

“Nilishakajua tu kama ikiwa najisikia muzuri sana maana yake ninakaribia kujisikia kuwa mwenye huzuni.”

“Najikazaka kukaza akili juu ya mambo yenye iko nafanyika leo, lakini wakati ingine mahangaiko ya mambo yenye ilishakapita ao yenye inawezatokea inakuwaka inanilemea.”

Ile ni maneno ya watu wenye wako na magonjwa ya akili. Uko napiganisha magumu ya vile? Ao mutu fulani mwenye unapendaka anajisikiaka vile?

Ukuwe hakika kama hauko weye peke. Watu wengi leo wako nateseka juu ya magonjwa ya akili yao wenyewe, ao ya watu wenye wanapendaka.

Kusema kweli, tukonaishi mu “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia,” zenye ziko naletea watu mahangaiko ya aina mbalimbali. (2 Timoteo 3:1) Uchunguzi moya ulionyesha kama, mu dunia yote mutu moya kati ya watu munane iko na magonjwa ya akili. Mu 2020, juu ya ugonjwa wa korona kuliongezeka watu karibu milioni 78 ku hesabu ya watu wenye wako na mahangaiko ya akili ao matatizo ya kushuka moyo.

Ni muzuri kujua hesabu ya watu wenye wako na mahangaiko ya akili ao matatizo ya kushuka moyo. Lakini, jambo ya maana zaidi ni kujua mambo yenye weye ao mutu fulani mwenye unapendaka munaweza kufanya juu mujisikie muzuri zaidi kadiri inawezekana.

Afya ya akili ni nini?

Ni hali yenye inafanya mutu ajisikie muzuri na akuwe na uwezo wa kufanya mambo. Mutu mwenye iko na afya ya muzuri ya akili anaweza kupiganisha mahangaiko ya kawaida, kutumika muzuri, na kujisikia kuwa mwenye furaha.

Matatizo ya akili . . .

  • HAIKO matokeo ya uzaifu wa mutu.

  • NI hali yenye inaleta mahangaiko ya mingi, na yenye inavuruga mawazo ya mutu, namna anajisikia, na tabia yake.

  • Inaweza kufanya ikuwe nguvu kwa mutu kuishi muzuri na wengine na kufanya ashindwe kutimiza mambo ya kawaida ya maisha ya kila siku.

  • Inaweza kupata watu wa miaka, desturi, rangi, kabila, dini yoyote. Inaweza kupata wenye walisoma ao wenye hawakusoma, na pia maskini ao matajiri.

Musaada kwa wale wenye wako na matatizo ya akili

Kama unatambua kuwa weye ao mutu fulani mwenye unapendaka anabadilisha tabia, haiko nalala ao kukula tena muzuri, amekuwa na mahangaiko, wasiwasi, ao huzuni yenye kukawia, inaweza kuwa muzuri kuona mutu mwenye anaweza kuwasaidia kujua tatizo ni nini na namna gani munaweza kuipiganisha. Sasa ni nani anaweza kusaidia?

Yesu Kristo, mutu mwenye hekima zaidi mwenye alishakaishi hapa ku dunia, alisemaka hivi: “Watu wenye afya ya muzuri hawana lazima ya munganga, lakini wagonjwa ndio wako na lazima yake.” (Matayo 9:12) Kama mutu mwenye iko na matatizo ya afya anapata matunzo yenye kufaa, anaweza kujisikia muzuri kwa kiasi fulani na anaweza kuwa na maisha yenye furaha. Ni jambo ya hekima kwa mutu wa vile kupata matunzo bila kukawia kama alama za ugonjwa ni za nguvu na zimekawia. a

Hata kama Biblia haiko kitabu ya matunzo, mashauri yenye iko ndani inaweza kukusaidia ukuwe na afya ya muzuri ya akili. Tafazali usome habari zenye kufuata zenye zinazungumuzia namna Biblia inaweza kutusaidia tupiganishe matatizo ya akili.

a Gazeti Munara wa Mulinzi haichochee watu wafuate aina fulani ya matunzo. Kila mutu anapaswa kuchunguza kwa uangalifu matunzo mbalimbali mbele aamue yeye mwenyewe matunzo yenye atakubali.