Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1 | Sala—“Mumutupie Mahangaiko Yenu Yote”

1 | Sala—“Mumutupie Mahangaiko Yenu Yote”

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mumutupie [Mungu] mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.” —1 PETRO 5:7.

Ile Iko na Maana Gani?

Yehova anatuomba tuzungumuze naye juu ya mizigo yoyote yenye iko buzito mu akili ao mu moyo wetu. (Zaburi 55:22) Tusikose kusali juu tunawaza kama magumu yetu ni ya mukubwa sana ao ni ya kidogo sana. Kama tu inatuhangaisha siye, inamuhangaisha pia Yehova. Kusali kwa Yehova ni jambo ya maana sana yenye tunapaswa kufanya kama tunapenda tukuwe na amani ya akili. —Wafilipi 4:6, 7.

Namna Gani ile Inaweza Kusaidia?

Wakati tuko napiganisha magonjwa ya akili, tunaweza kujisikia kuwa peke yetu kabisa. Wakati fulani watu wengine wanaweza kukosa kuelewa kabisa mambo yenye tuko napitia. (Mezali 14:10) Lakini wakati tunasali kwa Mungu na kumuambia waziwazi namna tuko najisikia, atatusikiliza, atajitia pa nafasi yetu, na atatuelewa. Yehova iko anatuona, anajua maumivu yetu, na mambo yenye iko natuhangaisha na anapenda tusali kwake juu ya jambo yoyote yenye iko natuhangaisha.—2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

Kuzungumuza na Yehova kupitia sala kunatusaidia tukuwe hakika zaidi kama anatuhangaikiaka. Ile inafanya tujisikie sawa mwandikaji moya wa zaburi mwenye alisali hivi: “Umeona mateso yangu; unajua taabu yangu nyingi.” (Zaburi 31:7) Kujua tu kama Yehova anaonaka mambo yenye iko natufikia inaweza kutusaidia tuvumilie magumu. Lakini, Yehova haishiake tu ku kuona mambo yenye iko natuhangaisha. Kuliko mutu mwingine yeyote, anaelewa mambo yenye iko natufikia na anatusaidia tupate mu Biblia mawazo yenye kutuliza na yenye kutia moyo.