Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Watu wa karibu dini zote kubwa wanaamini kama kuko nafsi yenye haiwezi kufa

HABARI KUBWA | BIBLIA INASEMA NINI JUU YA UZIMA NA KIFO?

Ulizo Lenye Kuhangaisha

Ulizo Lenye Kuhangaisha

KUKO mawazo mengi tofauti juu ya uzima na kifo. Watu fulani wanawaza kama kisha kufa wataendelea kuishi, pengine katika hali ingine ao mahali pengine. Wengine wanawaza kama watazaliwa tena ili kuishi katika hali ingine. Wengine tena wanawaza kama kifo ni mwisho wa mambo yote.

Unaweza kuwa na mawazo yako juu ya jambo hilo, kulingana na namna ulikomaa ao desturi yako. Kwa sababu mawazo kuhusu jambo lenye linatokea wakati mutu anakufa yako tofauti sana, kuko mutu fulani ao nafasi fulani kwenye tunaweza kupata majibu ya kweli na yenye kutegemeka kwa ulizo hilo lenye kuhangaisha?

Kwa miaka mingi sana, viongozi wa dini wamefundisha fundisho la kutokufa kwa nafsi ya mwanadamu. Watu wa karibu dini zote kubwa​—Wakristo, Wahindu, Wayahudi, Waislamu, na wengine​—wanaamini kama kuko nafsi yenye haiwezi kufa, ambayo inasemekana kwamba inaendelea kuishi katika makao ya roho kisha mutu kufa. Kwa upande mwengine, Wabuda wanaamini kama matokeo ya kuzaliwa upya mara nyingi ni kwamba, mutu anafikia kuwa katika hali ya bila mateso. Hali hiyo ya raha inaitwa Nirvana.

Kwa sababu ya mafundisho kama hayo, watu wengi katika dunia wamefikia kuamini kwamba kifo kinapatia watu nafasi ya kuishi katika ulimwengu mwingine. Kwa watu wengi, kifo ni hatua ya maana katika muzunguko wa maisha, na wanaona kama kifo ni mapenzi ya Mungu. Biblia inasema nini juu ya jambo hilo? Tafazali, soma habari yenye kufuata. Pengine jibu linaweza kukushangaza.