Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakati Ufalme wa Mungu utaanza kuwatawala, watu “watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”​—Zaburi 37:11.

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Biblia inaweza kukusaidia kupambana na mahangaiko?

Unaweza kujibu nini?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Pengine

Mambo Biblia inasema

‘Mumutupie [Mungu] mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’ (1 Petro 5:7) Biblia inakuhakikishia kwamba Mungu anaweza kukusaidia kupata kitulizo wakati unapata mahangaiko.

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Kupitia sala, unaweza kupata “amani ya Mungu” yenye inaweza kufanya mahangaiko yakuwe mwepesi.​—Wafilipi 4:6, 7.

  • Tena, kusoma Neno la Mungu kunaweza kukusaidia kupambana na mahangaiko.​—Mathayo 11:28-30.

Kuna siku mahangaiko yataisha?

Watu fulani wanaamini . . . kwamba mahangaiko na mikazo ni mambo ya kawaida katika maisha ya wanadamu, na wengine wanaamini kwamba mahangaiko yanaweza kuisha tu kisha mutu kufa. Wewe unawaza nini?

Mambo Biblia inasema

Mungu atamaliza mambo yote yenye kuleta mahangaiko. “Kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”​—Ufunuo 21:4.

Biblia inatufundisha tena nini?

  • Wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala wanadamu, watu wataishi katika amani na utulivu.​—Isaya 32:18.

  • Mahangaiko yenye hayako ya maana yatasahaulika.​—Isaya 65:17.