Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Luga Zetu za Leo Zilianzia Kwenye “Munara wa Babeli”?

Luga Zetu za Leo Zilianzia Kwenye “Munara wa Babeli”?

‘Yehova akawatawanya juu ya uso wote wa dunia kutoka huko, nao pole kwa pole wakaacha kulijenga lile jiji. Hiyo ndiyo sababu liliitwa jina lake Babeli, kwa sababu huko ndiko Yehova alikuwa amevuruga luga ya dunia yote.’​—Mwanzo 11:8, 9.

TUKIO hilo ambalo linazungumuziwa katika Biblia lilitokea kwelikweli? Je, watu walianza kuzungumuza luga mbalimbali mara moja, kama inavyoelezwa katika Biblia? Watu fulani hawakubali habari ya Biblia kuhusu namna luga za wanadamu zilivyoanza na kuenea duniani pote. Muandikaji mumoja anasema hivi: “Hadisi juu ya Munara wa Babeli ni moja kati ya hadisi zisizo na maana ambazo watu wanaeleza.” Hata mwalimu mumoja wa dini ya Kiyahudi aliita hadisi hiyo kuwa “jambo la upumbavu la kujaribu kueleza namna mataifa yalivyoanza.”

Sababu gani watu wanapinga habari ya Biblia juu ya Munara wa Babeli? Kwa kifupi, habari hiyo haipatane na mawazo fulani kuhusu namna luga zilivyoanza. Kwa mufano, watu fulani wenye elimu wanasema kwamba vikundi vya luga havikutokea mara moja lakini vilibadilika polepole kutokana na “luga moja ya kwanza kabisa.” Wengine wanaamini kwamba luga mbalimbali za mwanzoni zilikomaa zenyewe bila kutegemea luga zingine, kuanzia miguno ya sauti tu mupaka kuunda maneno mengi. Mawazo hayo na mawazo mengine yenye kupingana yamefanya watu wengi wakubaliane na Profesa Tecumseh Fitch, ambaye aliandika katika kitabu chake hivi: “Bado hatujapata majibu yenye kusadikisha kabisa.” (The Evolution of Language)

Ni mambo gani ambayo wachimbuaji wa vitu vya zamani na wachunguzi wamevumbua juu ya namna luga za wanadamu zilivyoanza na kufanya maendeleo Je, mambo ambayo wamevumbua yanaonyesha ukweli wa mawazo yote ambayo watu wanatoa? Ao, je, mambo ambayo wamevumbua yanaunga mukono habari ya Biblia kuhusu Munara wa Babeli? Kwanza, acheni tuchunguze kwa uangalifu habari hiyo ya Biblia.

HABARI HIYO ILITOKEA WAPI NA WAKATI GANI?

Biblia inasema kwamba muvurugo wa luga na kutawanyika kwa watu vilitokea katika ‘inchi ya Shinari,’ ambayo iliitwa baadaye Babiloni. (Mwanzo 11:2) Jambo hilo lilitokea wakati gani? Biblia inasema kwamba “dunia ilikuwa imegawanyika” katika siku za Pelegi, aliyezaliwa karibu miaka 250 mbele ya Abrahamu. Kwa hiyo, ni wazi kwamba matukio yaliyotendeka huko Babeli yalitendeka miaka 4200 hivi iliyopita.​—Mwanzo 10:25; 11:18-26.

Watu fulani wenye elimu wanawaza kwamba luga za sasa zilitokana na luga moja ya kwanza kabisa, ni kusema, luga ya asili ambayo walifikiri wanadamu walizungumuza karibu miaka 100000 iliyopita. * Wengine wanasema kwamba luga za leo zilitokana na luga mbalimbali za kwanza ambazo zilizungumuzwa karibu miaka 6000 iliyopita. Lakini, watu wenye elimu ya luga wanafanya nini ili kujua namna luga za zamani ambazo zimepotea zilivyofanya maendeleo? Gazeti moja linasema kwamba “hilo ni jambo ngumu. Tofauti na wanabiolojia, watu wenye elimu ya luga hawana mabaki ya vitu vya zamani ili kuwaongoza kujua mambo ya wakati uliopita.” Gazeti hilo linaongeza kwamba mutu mumoja mwenye elimu ya luga anayeamini kwamba luga zilifanya maendeleo anafikia maamuzi yake kupitia “hesabu za kuwazia-wazia tu.” (Economist)

Hata hivyo, “maandishi ya zamani” yanapatikana. Maandishi hayo ni gani, na yanafunua nini kuhusu namna luga za wanadamu zilivyoanza? Kitabu kimoja kinaeleza hivi: “Maandishi ya zamani zaidi ya luga iliyoandikwa, ambayo watu wanaweza kutumainia kupata, ni yale ya tangu miaka 4000 ao 5000 hivi iliyopita.” (The New Encyclopædia Britannica) Ni wapi wachimbuaji wa vitu vya zamani walipata “maandishi hayo ya zamani,” ao “maandishi ya luga iliyoandikwa”? Walipata maandishi hayo katika Mesopotamia ya chini, mahali ambapo kulikuwa Shinari ya zamani. * Kwa hiyo, ushuhuda unaopatikana wa vitu vya zamani unapatana na mambo ya hakika ambayo yanazungumuziwa katika Biblia.

LUGA TOFAUTI-TOFAUTI, NAMNA TOFAUTI​-TOFAUTI ZA KUFIKIRI

Habari hiyo ya Biblia inasema kwamba kwenye Munara wa Babeli, Mungu ‘alivuruga luga yao huko ili wasiweze kusikilizana luga.’ (Mwanzo 11:7) Matokeo ni kwamba, wajenzi “wakaacha kulijenga lile jiji” la Babeli na wakatawanyika “juu ya uso wote wa dunia.” (Mwanzo 11:8, 9) Kwa hiyo, Biblia haiseme kwamba luga zote za leo zilitokana na “luga moja ya asili.” Lakini, inaeleza kutokea kwa gafula kwa luga mupya mbalimbali ambazo labda zilikuwa tayari zimefanya maendeleo, kila moja ikiwa na uwezo wa kueleza vizuri mawazo ya mwanadamu na namna anavyojisikia moyoni na kila moja ikiwa tofauti na luga zingine.

Kipande cha udongo kilicho na maandishi ya kikabari, kutoka Mesopotamia, cha tangu mileani ya tatu mbele ya kuzaliwa kwa Yesu

Tuseme nini kuhusu vikundi vya luga vinavyopatikana duniani leo? Je, vikundi hivyo vya luga vinafanana ao viko tofauti? Lera Boroditsky, mwanasayansi wa mambo ya akili, aliandika hivi: “Watu wenye elimu ya luga walipochunguza kwa undani luga zilizo duniani leo (7000 ao zaidi, ni luga chache tu kati ya hizo ndizo zilizochunguzwa), tofauti nyingi ambazo hazikutazamiwa ziliweza kujitokeza.” Kwa kweli, ijapokuwa luga kubwa na luga ndogo-ndogo za kikundi kimoja cha luga, kama vile Otetela na Lingala zinazozungumuzwa katika inchi yetu ya Congo Kinshasa, zinaweza kufanana, luga hizo ni tofauti kabisa na luga za kikundi kingine, kama vile Kifaransa.

Luga zinaongoza namna watu wanavyofikiri juu ya mambo yanayowazunguka na namna wanavyoeleza mambo hayo, kwa mufano mambo kama vile, rangi, uwingi, mahali ambapo mutu anapatikana na mahali ambapo anaelekea. Kwa mufano, katika luga moja mutu anaweza kusema, “Kuna mududu kwenye mukono wako wa kuume.” Lakini katika luga nyingine, mutu anaweza kusema, “Kuna mududu kwenye mukono wako wa kusini-mangaribi.” Kwa kifupi, tofauti kama hizo zinaweza kuvuruga mutu. Haishangaze kwamba ilikuwa vigumu kwa wajenzi wa Munara wa Babeli kuendelea na ujenzi wao.

LUGA YA ZAMANI ILIKUWA MIGUNO YA SAUTI AO LUGA YENYE MANENO MENGI?

Luga ya kwanza kabisa ya wanadamu ilikuwa namna gani? Biblia inaeleza kwamba mwanaume wa kwanza, Adamu, alikuwa na uwezo wa kuunda maneno mapya wakati aliwapatia wanyama wote na ndege majina. (Mwanzo 2:20) Adamu aliunda pia mashairi (maneno yaliyopangwa kwa utaratibu fulani) ili kuonyesha upendo kwa Eva bibi yake, na Eva alieleza waziwazi mambo ambayo Mungu aliagiza na matokeo mabaya ambayo wangepata ikiwa wanakosa kumutii Mungu. (Mwanzo 2:23; 3:1-3) Kwa hiyo, luga ya kwanza kabisa iliwawezesha wanadamu kupashana habari vizuri na kujieleza kwa kuunda maneno mengine mapya.

Muvurugo wa luga kwenye Munara wa Babeli haukuwawezesha tena wajenzi wa Munara huo kuchanganya uwezo wao wa kiakili na kimwili ili kutimiza kazi hiyo. Lakini, luga zao mupya, kama vile luga ya kwanza kabisa, zilikuwa na maneno mengi. Kwa mamia machache ya miaka tu, watu walijenga miji mikubwa, waliunda majeshi yenye nguvu, na walifanya biashara ya kimataifa. (Mwanzo 13:12; 14:1-11; 37:25) Je, wangefanya maendeleo yote hayo bila kutumia luga iliyo na maneno mengi na mupangilio muzuri na kisarufi? Kulingana na Biblia, luga ya kwanza kabisa ya wanadamu na luga zingine zilizotokana na muvurugo kwenye Munara wa Babeli, hazikuwa miguno ya sauti tu na maneno ya chini-chini, lakini zilikuwa luga zenye maneno mengi.

Wachunguzi wa leo wanaunga mukono wazo hilo. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Kila kikundi cha watu ambacho kimechunguzwa, iwe bado kinaishi kulingana na desturi za ‘zamani’, kina luga yenye kufanya maendeleo, na mambo ya pekee yanayolingana na ya luga za mataifa ambayo yanaonwa kuwa ‘yenye kusirimuka.’” (The Cambridge Encyclopedia of Language) Vilevile, katika kitabu chake kimoja, Steven Pinker Profesa wa Chuo Kikubwa cha Harvard, anaeleza hivi: “Hakuna luga zisizo na maendeleo.” (The Language Instinct)

LUGA YA WAKATI UJAO

Kisha kuchunguza miaka ya “maandishi ya zamani” na mahali ambapo yalipatikana, tofauti kubwa kati ya vikundi vya luga, na mambo ya pekee ya luga za zamani, ni maamuzi gani tunaweza kufikia? Watu wengi wanafikia uamuzi wa kwamba habari ya Biblia kuhusu mambo yaliyotokea kwenye Munara wa Babeli ni maelezo yenye kutegemeka.

Biblia inatueleza kwamba Yehova alivuruga luga za watu kwenye Munara wa Babeli kwa sababu walimuasi. (Mwanzo 11:4-7) Hata hivyo, anaahidi ‘kuwapa watu luga safi, ili wote waliitie jina la Yehova, wamutumikie bega kwa bega.’ (Sefania 3:9) Hiyo ‘luga safi,’ ni kusema, kweli ya Neno la Mungu, inaunganisha leo watu wa dunia yote. Ni jambo lenye kueleweka kwamba wakati ujao Mungu ataunganisha wanadamu wote kwa kuwapatia luga moja, na hivyo kuondoa muvurugo uliotokana na Munara wa Babeli.

^ Mara nyingi mawazo ya watu kuhusu luga yanaonyesha kwamba wanadamu walitokana na viumbe vilivyo kama nyani ambavyo viligeuka​-geuka mupaka kufikia kuwa wanadamu. Ili kuchunguza mawazo kama hayo, soma ukurasa wa 27-29 wa broshua Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ Wachimbuaji wa vitu vya zamani walivumbua ndani ya udongo, karibu na eneo la Shinari, minara mbalimbali ya hekalu yenye vipandio inayofanana na piramidi. Biblia inasema kwamba wajenzi wa Munara wa Babeli walitengeneza matofali, wala si majiwe, na walitumia lami kama saruji ao simenti. (Mwanzo 11:3, 4) Kitabu kimoja kinasema kwamba katika Mesopotamia, majiwe “hayakupatikana kwa urahisi ao hayakuwa kabisa,” lakini lami ilipatikana kwa uwingi. (The New Encyclopædia Britannica)