Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPATA FAIDA WAKATI UNASOMA BIBLIA?

Namna Gani Biblia Inaweza Kufanya Maisha Yangu Yakuwe Muzuri Zaidi?

Namna Gani Biblia Inaweza Kufanya Maisha Yangu Yakuwe Muzuri Zaidi?

Biblia iko tofauti na vitabu vingine vyote. Iko na mashauri kutoka kwa Muumbaji wetu. (2 Timotheo 3:16) Ujumbe wa Biblia unaweza kuwa na matokeo makubwa juu yetu. Kwa kweli, Biblia inasema hivi: “Neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu.” (Waebrania 4:12) Biblia iko na nguvu ya kufanya maisha yetu yakuwe ya muzuri zaidi katika njia mbili za maana: kwa kututolea muongozo katika maisha yetu ya kila siku sasa, na kwa kutusaidia kujua Mungu na ahadi zake.—1 Timotheo 4:8; Yakobo 4:8.

Inaweza kufanya maisha yako yakuwe muzuri zaidi leo. Biblia inaweza kukusaidia katika maisha yako. Inatoa mashauri juu ya mambo yenye kufuata.

Katika Asia bibi na bwana fulani vijana walifurahia sana faida ya mashauri ya Biblia. Kama bibi na bwana wengi wenye kufunga ndoa hivi karibuni, ilikuwa vigumu kwa kila mumoja wao kuzoea tabia ya mwengine na kuzungumuza waziwazi. Lakini walianza kutumikisha mambo yenye walikuwa wanasoma katika Biblia. Walipata matokeo gani? Bwana huyo mwenye kuitwa Vicent, anasema hivi: “Mambo yenye nilisoma katika Biblia yalinisaidia kushugulikia matatizo katika ndoa yetu kwa upendo. Kuishi kulingana na mashauri ya Biblia kumetusaidia kuwa na maisha yenye furaha.” Bibi yake, Annalou, anakubali kwa kusema hivi: “Kusoma mifano mbalimbali katika Biblia kulitusaidia. Sasa ninafurahia ndoa yetu na mambo yenye tumepanga kutimiza katika maisha.”

Inaweza kukusaidia umujue Mungu. Zaidi ya mambo yenye alisema juu ya ndoa, Vicent anasema tena hivi: “Kupitia kusoma Biblia, ninajisikia kuwa niko karibu zaidi na Yehova kuliko zamani.” Maneno hayo ya Vicent yanakazia jambo la maana sana, ni kusema, Biblia inaweza kukusaidia umujue Mungu. Kwa kusoma Biblia, mashauri ya Mungu yatakuletea faida, lakini utaona pia kwamba unaweza kufikia kumujua kama rafiki. Tena, utaona mambo mbalimbali yenye anafunua juu ya wakati muzuri wenye kuja, wakati huo utaweza kufurahia “uzima ulio wa kweli” ambao utaendelea milele. (1 Timotheo 6:19) Hakuna kitabu kingine chenye kinaweza kukutolea jambo hilo.

Ikiwa unaanza kusoma Biblia na kuendelea kufanya hivyo, unaweza kupata faida hizo, ni kusema, utakuwa na maisha ya muzuri zaidi leo na utafikia kumujua Mungu. Lakini, wakati unasoma Biblia unaweza kujiuliza maulizo mengi. Na wakati unakuwa na maulizo, kumbuka mufano muzuri wa ofisa Mwethiopia mwenye aliishi kumepita miaka 2000. Alikuwa na maulizo mengi juu ya Biblia. Wakati Filipo alimuuliza ikiwa anaelewa mambo yenye alikuwa anasoma, alimujibu hivi: ‘Kwa kweli, ninawezaje kuelewa, mutu fulani asiponiongoza?’ * Kisha alikuwa tayari kukubali musaada kutoka kwa Filipo, mwanafunzi wa Yesu wa wakati wa mitume, mwenye alikuwa tayari mwalimu muzuri wa Biblia. (Matendo 8:30, 31, 34) Wewe pia kama unapenda kujua mambo mengi zaidi juu ya Biblia, tunakualika ujaze fomu yenye kuwa kwenye adresi yetu ya Internete jw.org ao uandikie adresi yenye kuwa katika gazeti hili. Unaweza pia kutafuta Mashahidi wa Yehova wenye kuwa karibu na mahali unaishi ao unaweza kutembelea Jumba la Ufalme lenye kuwa katika eneo lenu. Sababu gani usianze kusoma Biblia leo na kuacha ikusaidie kuwa na maisha ya muzuri zaidi?

Ikiwa unajiuliza kama unaweza kutumainia kabisa Biblia, tafazali angalia video fupi yenye kichwa, Namna Gani Tunaweza Kuwa Hakika Kama Biblia Inasema Kweli? Unaweza kuipata kwa kutumia chombo cha kusoma alama yenye kuwa pembeni ao kwa kufungua jw.org, kwenye kichwa VICHAPO > VIDEO

^ fu. 8 Ili kupata mashauri ya Biblia juu ya mambo mengine, fungua adresi yetu ya Internete, jw.org/sw. Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA.

^ fu. 11 Soma pia habari “Ni Tatizo Ndogo Tu la Kukosa Kuelewa?” yenye kuwa katika gazeti hili.