Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Thomas Jackson/​Stone via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Kupata Tumaini mu 2024​—⁠Biblia Inasema Nini?

Kupata Tumaini mu 2024​—⁠Biblia Inasema Nini?

 Watu wengi wanaona kama hakuna namna ya kupambana na magumu yenye kuwa mu dunia mu 2024. Lakini, tunaweza kupata tumaini juu ya wakati wenye kuya. Tutaipata wapi?

Biblia Inatupatia Tumaini

 Biblia inaahidi kama Mungu atamaliza magumu yenye inafanya watu wakose tumaini. Hivi karibuni, Mungu “atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—Ufunuo 21:4.

  •   Juu ya kujua mambo mingi juu ya mambo yenye Biblia inaahidi juu ya wakati wenye kuya, soma habari “Tumaini Bora la Wakati Ujao.”

Namna Biblia inaweza kukusaidia leo

 Biblia inatupatia tumaini juu ya wakati wenye kuya, na ile tumaini inafanya tusivunjike moyo na tukuwe hakika kama mambo itakuwa muzuri. (Waroma 15:13) Mashauri yenye Biblia inatupatia inaweza pia kutusaidia kupiganisha magumu yenye tuko nayo leo, sawa vile umaskini, ukosefu wa haki, na magonjwa.

 Fanya mwaka wa 2024 kuwa mwaka muzuri kwa ajili yako na familia yako. Ujifunze namna Biblia inaweza kukusaidia. Bila kulipa na kwa njia ya mazungumuzo, pima kujifunza na siye Biblia. Utaona namna Biblia inaweza kukupatia “mawazo ya amani,” na “wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini.”​—Yeremia 29:11.