Hamia kwenye habari

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Kuwa na Familia Yenye Furaha?

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Kuwa na Familia Yenye Furaha?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Hapa kuna mashauri kadhaa yanayotegemea Biblia ambayo yamesaidia mamilioni ya wanaume na wanawake kuwa na familia yenye furaha:

  1.   Halalisha ndoa yako. Msingi wa kuwa na familia yenye furaha ni kufunga ndoa halali ambayo haipaswi kuvunjwa.​—Mathayo 19:4-6.

  2.   Mpendane na kuheshimiana. Hili linatia ndani kumtendea mwenzi wako kama vile tu wewe ungependa kutendewa.​—Mathayo 7:12; Waefeso 5:25, 33.

  3.   Epuka maneno makali. Zungumza kwa upole hata kama mwenzi wako amesema au kufanya jambo fulani lenye kuumiza. (Waefeso 4:31, 32) Kama vile Biblia isemavyo katika andiko la Methali 15:1: “Jibu, linapokuwa la upole, hugeuza ghadhabu, lakini neno linaloumiza hufanya hasira ipande.”

  4.   Uwe mwaminifu kwa mwenzi wako. Mwonyeshe mahaba mwenzi wako tu. (Mathayo 5:28) Biblia inasema: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi.”​—Waebrania 13:4.

  5.   Walee watoto wako kwa upendo. Usiendekeze wala kuwa mkatili.​—Methali 29:15; Wakolosai 3:21.