Kwa Waefeso 5:1-33

  • Usemi na mwenendo safi (1-5)

  • Tembeeni kama watoto wa nuru (6-14)

  • Mjazwe roho (15-20)

    • Tumieni vizuri kabisa wakati wenu (16)

  • Ushauri kwa waume na wake (21-33)

5  Kwa hiyo, iweni waigaji wa Mungu,+ kama watoto wapendwa,  na mwendelee kutembea katika upendo,+ kama vile Kristo pia alivyotupenda sisi*+ na kujitoa mwenyewe kwa ajili yetu* kuwa toleo na dhabihu yenye harufu tamu kwa Mungu.+  Uasherati* na kila namna ya ukosefu wa usafi au pupa visitajwe kamwe miongoni mwenu,+ kama inavyowafaa watu watakatifu;+  wala mwenendo wa aibu wala maneno ya kipumbavu wala mizaha michafu+—mambo yasiyofaa—badala yake, kutoa shukrani.+  Kwa maana mnajua hili, nanyi mnalitambua wenyewe, kwamba hakuna mwasherati*+ au mtu asiye safi au mtu mwenye pupa,+ maana yake mtu anayeabudu sanamu, aliye na urithi wowote katika Ufalme wa Kristo na wa Mungu.+  Mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa maana ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wa kutotii kwa sababu ya mambo hayo.  Kwa hiyo, msishirikiane nao;  kwa kuwa wakati fulani mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru+ kuhusiana na Bwana.+ Endeleeni kutembea kama watoto wa nuru,  kwa maana tunda la nuru lina kila namna ya wema na uadilifu na kweli.+ 10  Endeleeni kuhakikisha jambo linalokubalika+ kwa Bwana; 11  na mwache kushiriki katika matendo yasiyozaa matunda, ambayo ni ya giza;+ badala yake, myafunue jinsi yalivyo. 12  Kwa maana mambo wanayotenda katika siri ni aibu hata kuyataja. 13  Basi mambo yote yanayofunuliwa yanawekwa wazi* na nuru, kwa maana kila jambo linalowekwa wazi ni nuru. 14  Kwa hiyo, inasemwa: “Amka, wewe unayelala usingizi, na ufufuke kutoka kwa wafu,+ na Kristo atakuangazia.”+ 15  Basi endeleeni kuangalia sana jinsi mnavyotembea, si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima, 16  mkiutumia vizuri kabisa wakati wenu,*+ kwa sababu siku hizi ni zenye uovu. 17  Kwa hiyo acheni kuwa watu wasio na akili, bali endeleeni kuyafahamu mapenzi ya Yehova.*+ 18  Pia, msilewe divai,+ ambayo ina upotovu,* bali endeleeni kujazwa roho. 19  Mkizungumza kati yenu* kwa zaburi, sifa kwa Mungu, na nyimbo za kiroho, mkiimba+ na kupiga muziki+ katika mioyo yenu kwa Yehova,*+ 20  sikuzote mkimtolea shukrani+ Mungu na Baba yetu kwa ajili ya mambo yote katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo.+ 21  Jitiisheni kila mmoja kwa mwenzake+ katika kumwogopa Kristo. 22  Wake na wajitiishe kwa waume zao+ kama kwa Bwana, 23  kwa sababu mume ni kichwa cha mke wake+ kama vile Kristo alivyo kichwa cha kutaniko,+ yeye akiwa mwokozi wa mwili huu. 24  Kwa kweli, kama vile kutaniko linavyojitiisha kwa Kristo, wanawake pia wanapaswa kujitiisha kwa waume zao katika mambo yote. 25  Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu,+ kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake,+ 26  ili alitakase, akilisafisha na kuliosha kwa maji kupitia neno,+ 27  ili kujipa mwenyewe kutaniko likiwa na fahari, bila doa au kunyanzi au lolote kati ya mambo hayo,+ bali likiwa takatifu na bila dosari.+ 28  Vivyo hivyo, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Mwanamume anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe, 29  kwa maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake, bali huulisha na kuutunza, kama vile Kristo anavyolitendea kutaniko, 30  kwa kuwa sisi ni viungo vya mwili wake.+ 31  “Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana* na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”+ 32  Siri hii takatifu+ ni kubwa. Sasa ninazungumza kuhusu Kristo na kutaniko.+ 33  Hata hivyo, kila mtu kati yenu anapaswa kumpenda mke wake+ kama anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “ninyi.”
Au labda, “yenu.”
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “yanakaripiwa.”
Tnn., “mkijinunulia wakati uliowekwa.”
Au “haina adabu.”
Au labda, “mkijizungumzia.”
Au “atabaki.”