Methali 15:1-33

  • Jibu la upole hutuliza hasira (1)

  • Macho ya Yehova yako kila mahali (3)

  • Sala ya mtu mnyoofu humfurahisha Mungu (8)

  • Mipango huvunjika watu wasiposhauriana (22)

  • Tafakari kabla ya kujibu (28)

15  Jibu la upole* hutuliza hasira,+Lakini neno kali* huchochea hasira.+   Ulimi wa mwenye hekima hutumia vizuri ujuzi,+Lakini kinywa cha mpumbavu hububujika ujinga.   Macho ya Yehova yako kila mahali,Yakiwaangalia waovu na wema.+   Ulimi mtulivu* ni mti wa uzima,+Lakini maneno yaliyopotoka hukatisha tamaa.*   Mjinga hudharau nidhamu ya baba yake,+Lakini mwerevu hukubali kurekebishwa.*+   Nyumba ya mwadilifu ina hazina tele,Lakini mazao* ya mwovu humletea taabu.+   Midomo ya wenye hekima hueneza ujuzi,+Lakini moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.+   Dhabihu ya waovu humchukiza Yehova,+Lakini sala ya wanyoofu humfurahisha Yeye.+   Yehova huchukia njia ya mwovu,+Lakini humpenda mtu anayefuatia uadilifu.+ 10  Nidhamu huonekana kuwa mbaya* kwa mtu anayeiacha njia,+Lakini yeyote anayechukia karipio atakufa.+ 11  Kaburi* na mahali pa maangamizi* viko wazi kabisa machoni pa Yehova.+ Sembuse mioyo ya wanadamu!+ 12  Mtu mwenye dhihaka hampendi anayemrekebisha.*+ Hatatafuta ushauri kutoka kwa wenye hekima.+ 13  Moyo wenye shangwe hufanya uso uchangamke,Lakini maumivu ya moyo huiponda roho.+ 14  Moyo wenye uelewaji hutafuta ujuzi,+Lakini kinywa cha wapumbavu hula* ujinga.+ 15  Siku zote za mtu anayeteseka ni mbaya,+Lakini mtu aliye na moyo mchangamfu* huwa na karamu daima.+ 16  Ni afadhali kuwa na vichache na kumwogopa Yehova+Kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na mahangaiko.*+ 17  Ni afadhali kula mboga za majani mahali penye upendo+Kuliko kula ng’ombe dume aliyenoneshwa* mahali penye chuki.+ 18  Mtu mwenye hasira kali huchochea mzozo,+Lakini mtu asiyekasirika upesi hutuliza ugomvi.+ 19  Njia ya mvivu ni kama uzio wa miiba,+Lakini kijia cha wanyoofu ni kama barabara iliyosawazika.+ 20  Mwana mwenye hekima humfanya baba yake ashangilie,+Lakini mtu mpumbavu humdharau mama yake.+ 21  Mtu asiye na busara* hufurahia ujinga,+Lakini mtu mwenye utambuzi huenda mbele moja kwa moja.+ 22  Mipango huvunjika watu wasiposhauriana,*Lakini mambo hufanikiwa kupitia washauri wengi.+ 23  Mtu hushangilia anapotoa jibu linalofaa,*+Na neno linalosemwa wakati unaofaa—ni jema sana!+ 24  Kwa mwenye ufahamu kijia cha uzima huelekea juu,+Ili kumwepusha na Kaburi* lililo chini.+ 25  Yehova ataibomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi,+Lakini ataulinda mpaka wa mjane.+ 26  Yehova huchukia njama za mtu mwovu,+Lakini maneno yanayopendeza ni safi Kwake.+ 27  Mtu anayepata faida isiyo ya haki huwaletea taabu* watu wa nyumba yake mwenyewe,+Lakini anayechukia rushwa ataendelea kuishi.+ 28  Moyo wa mwadilifu hutafakari kabla ya kujibu,*+Lakini kinywa cha waovu hububujika mambo mabaya. 29  Yehova yuko mbali sana na waovu,Lakini huisikia sala ya waadilifu.+ 30  Macho yanayong’aa* huufanya moyo ushangilie;Habari njema huitia nguvu mifupa.*+ 31  Mtu anayesikiliza karipio la uzimaHutulia miongoni mwa wenye hekima.+ 32  Yeyote anayekataa nidhamu anaudharau uhai wake,*+Lakini yeyote anayesikiliza karipio hupata uelewaji.*+ 33  Kumwogopa Yehova ni mazoezi ya kupata hekima,+Na kabla ya utukufu kuna unyenyekevu.+

Maelezo ya Chini

Au “linaloumiza.”
Au “tulivu.”
Au “Ulimi unaoponya.”
Tnn., “huiponda roho.”
Au “karipio.”
Au “mapato.”
Au “kali.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “na Abadoni.”
Au “anayemkaripia.”
Au “hufuatia.”
Au “mzuri.”
Au “vurugu.”
Tnn., “aliyelishwa kwenye hori.”
Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
Au “watu wasipokuwa na mazungumzo ya siri.”
Tnn., “hushangilia jibu la kinywa chake.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “aibu.”
Au “hufikiria kwa uangalifu jinsi ya kujibu; hufikiria kabla ya kuongea.”
Au “Kumtupia mtu jicho kwa uchangamfu.”
Tnn., “huinenepesha mifupa.”
Au “anaidharau nafsi yake.”
Tnn., “moyo.”