Kitabu cha Pili cha Wafalme 13:1-25

  • Yehoahazi, mfalme wa Israeli (1-9)

  • Yehoashi, mfalme wa Israeli (10-13)

  • Elisha apima bidii ya Yehoashi (14-19)

  • Kifo cha Elisha; mifupa yake yamfufua mtu (20, 21)

  • Unabii wa mwisho wa Elisha watimizwa (22-25)

13  Katika mwaka wa 23 wa utawala wa Yehoashi+ mwana wa Ahazia+ mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu+ akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 17.  Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, na kuendelea kutenda dhambi ya Yeroboamu mwana wa Nebati aliyosababisha Waisraeli kutenda.+ Hakugeuka na kuiacha.  Kwa hiyo hasira ya Yehova+ ikawaka dhidi ya Waisraeli,+ akawatia mikononi mwa Mfalme Hazaeli+ wa Siria na mikononi mwa Ben-hadadi+ mwana wa Hazaeli siku zao zote.  Baada ya muda Yehoahazi akamsihi Yehova amwonyeshe kibali,* naye Yehova akamsikiliza, kwa maana alikuwa ameona jinsi mfalme wa Siria alivyowakandamiza Waisraeli.+  Basi Yehova akawapa Waisraeli mwokozi+ ili awaokoe kutoka mikononi mwa Wasiria, na Waisraeli wakakaa katika nyumba zao kama awali.*  (Hata hivyo, hawakuacha dhambi ya nyumba ya Yeroboamu aliyosababisha Waisraeli kutenda.+ Waliendelea kutenda* dhambi hiyo, na mti mtakatifu*+ ukaendelea kusimama huko Samaria.)  Yehoahazi akabaki tu na jeshi lenye wapanda farasi 50, magari 10 ya vita, na wanajeshi 10,000 wanaotembea kwa miguu kwa sababu mfalme wa Siria alikuwa amewaangamiza,+ aliwakanyaga-kanyaga kama mavumbi wakati wa kupura.+  Na mambo mengine katika historia ya Yehoahazi, mambo yote aliyofanya na ukuu wake, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli?  Kisha Yehoahazi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake huko Samaria;+ na Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake. 10  Katika mwaka wa 37 wa utawala wa Mfalme Yehoashi wa Yuda, Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 16. 11  Akaendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, hakuacha kutenda dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati alizosababisha Waisraeli kutenda.+ Aliendelea kutenda* dhambi hizo. 12  Na mambo mengine katika historia ya Yehoashi, mambo yote aliyofanya na ukuu wake na jinsi alivyopigana na Mfalme Amazia wa Yuda,+ je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 13  Kisha Yehoashi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake, na Yeroboamu*+ akaketi kwenye kiti chake cha ufalme. Naye Yehoashi akazikwa huko Samaria pamoja na wafalme wa Israeli.+ 14  Sasa Elisha+ alipougua ugonjwa ambao hatimaye ulisababisha kifo chake, Yehoashi mfalme wa Israeli alishuka kwenda kwake na kumlilia akisema: “Baba yangu, baba yangu! Gari la vita la Israeli na wapanda farasi wake!”+ 15  Ndipo Elisha akamwambia: “Chukua upinde na mishale.” Basi akachukua upinde na mishale. 16  Kisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Shika upinde wako.” Basi akashika upinde wake, halafu Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme. 17  Kisha akasema: “Fungua dirisha la upande wa mashariki.” Basi akalifungua. Elisha akasema: “Piga mshale!” Basi akapiga mshale. Sasa akasema: “Mshale wa ushindi* wa Yehova, mshale wa ushindi* dhidi ya Siria! Utapiga* Siria huko Afeki+ mpaka uiangamize kabisa.” 18  Akaendelea kusema: “Chukua mishale,” naye akaichukua. Kisha Elisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Piga ardhi.” Basi akapiga ardhi mara tatu halafu akaacha. 19  Ndipo yule mtu wa Mungu wa kweli akamkasirikia sana na kumwambia: “Ulipaswa kuipiga ardhi mara tano au mara sita! Kama ungefanya hivyo, ungeipiga Siria mpaka uiangamize, lakini sasa utaipiga Siria mara tatu tu.”+ 20  Baada ya hayo, Elisha akafa na kuzikwa. Kulikuwa na makundi ya wavamizi+ ya Wamoabu yaliyokuwa yakija nchini mwanzoni mwa mwaka.* 21  Wanaume fulani walipokuwa wakimzika mtu, waliona kundi la wavamizi, kwa hiyo wakamtupa mara moja mtu huyo ndani ya kaburi la Elisha na kukimbia. Mtu huyo alipogusa mifupa ya Elisha, akafufuka+ na kusimama. 22  Sasa Mfalme Hazaeli+ wa Siria aliwakandamiza Waisraeli+ sikuzote za utawala wa Yehoahazi. 23  Hata hivyo, Yehova akawaonyesha kibali na rehema+ na kuwajali kwa sababu ya agano lake na Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+ Hakutaka kuwaangamiza, naye hajawatupa mbali kutoka mbele zake* mpaka leo. 24  Mfalme Hazaeli wa Siria alipokufa, Ben-hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake. 25  Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akayachukua tena majiji ambayo Ben-hadadi mwana wa Hazaeli alikuwa ameyachukua vitani kutoka kwa Yehoahazi baba yake. Yehoashi alimshinda Ben-hadadi mara tatu,+ naye akayakomboa majiji ya Israeli.

Maelezo ya Chini

Au “akautuliza uso wa Yehova.”
Yaani, kwa amani na usalama.
Tnn., “Aliendelea kutembea katika.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “Alitembea katika.”
Yaani, Yeroboamu wa Pili.
Au “wokovu.”
Au “wokovu.”
Au “Utaishinda.”
Tnn., “mwaka unapoingia,” inawezekana ni wakati wa masika.
Tnn., “kutoka kwenye uwepo wake.”