Barua ya Pili kwa Wakorintho 5:1-21

  • Kuvaa makao ya kimbingu (1-10)

  • Huduma ya upatanisho (11-21)

    • Kiumbe kipya (17)

    • Mabalozi wa Kristo (20)

5  Kwa maana tunajua kwamba nyumba yetu ya kidunia, hema hili, likiharibiwa,*+ tutapata jengo kutoka kwa Mungu, nyumba ya milele mbinguni, ambayo haijajengwa kwa mikono.+  Kwa maana tunaugua kwelikweli katika nyumba hii,* tukitamani sana kuvaa ile yetu* kutoka mbinguni,*+  ili kwamba tutakapoivaa, hatutapatikana tukiwa uchi.  Kwa kweli, sisi tulio katika hema hili tunaugua, tukilemewa kwa sababu hatutaki kuuvua huu, bali tunataka kuuvaa ule mwingine,+ ili uhai ukimeze kile kinachoweza kufa.+  Basi yule aliyetutayarisha kwa ajili ya jambo hili ni Mungu,+ ambaye alitupatia roho kama rehani ya kile kitakachokuja.*+  Basi sikuzote sisi tuna uhodari mwingi na tunajua kwamba tukiwa na makao yetu katika mwili, hatupo mahali alipo Bwana,+  kwa maana tunatembea kwa imani, si kwa kuona.  Lakini sisi tuna uhodari mwingi na tungependelea tusiwepo katika mwili bali tuyafanye makao yetu pamoja na Bwana.+  Basi iwe ni nyumbani pamoja naye au tusipokuwa pamoja naye, lengo letu ni kukubalika kwake. 10  Kwa maana lazima sisi sote tusimame* mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate malipo kulingana na mambo aliyotenda akiwa katika mwili, yawe mema au mabaya.*+ 11  Kwa hiyo, kwa kuwa tunajua kumwogopa Bwana, tunaendelea kuwashawishi watu, lakini tunafahamika vizuri* kwa Mungu. Hata hivyo, ninatumaini kwamba tunafahamika vizuri* pia kwa dhamiri zenu. 12  Hatujipendekezi wenyewe tena kwenu, bali tunawapa kichocheo cha kujisifu kuhusiana nasi, ili muweze kujibu wale wanaojisifu kuhusu sura ya nje+ bali si kuhusu yaliyo moyoni. 13  Kwa maana ikiwa tulikuwa tumerukwa na akili,+ ilikuwa ni kwa ajili ya Mungu; ikiwa tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu. 14  Kwa maana upendo alio nao Kristo hutuchochea, kwa sababu tumefikia uamuzi huu, kwamba mtu mmoja alikufa kwa ajili ya wote;+ hivyo basi, wote walikuwa wamekufa. 15  Naye alikufa kwa ajili ya wote ili wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe,+ bali kwa ajili ya yule aliyekufa kwa ajili yao na kufufuliwa. 16  Basi tangu sasa hatumjui mtu yeyote kulingana na maoni ya kimwili.+ Hata kama wakati fulani tulimjua Kristo kulingana na mwili, kwa hakika hatumjui tena kwa njia hiyo.+ 17  Kwa hiyo, ikiwa yeyote yuko katika muungano na Kristo, yeye ni kiumbe kipya;+ mambo ya zamani yalipitilia mbali; tazama! mambo mapya yamekuja kuwapo. 18  Lakini mambo yote yametoka kwa Mungu, aliyetupatanisha sisi kwake mwenyewe kupitia Kristo+ na kutupatia huduma ya upatanisho,+ 19  yaani, kwamba Mungu kupitia Kristo alikuwa akiupatanisha ulimwengu kwake mwenyewe,+ bila kuwahesabia makosa yao,+ naye alitukabidhi ujumbe wa upatanisho.+ 20  Kwa hiyo sisi ni mabalozi+ walio badala ya Kristo,+ kana kwamba Mungu alikuwa akisihi kupitia sisi. Kama walio badala ya Kristo, tunaomba: “Mpatanishwe na Mungu.” 21  Yule ambaye hakujua dhambi+ alimfanya kuwa dhambi* kwa ajili yetu, ili kupitia yeye tuwe uadilifu wa Mungu.+

Maelezo ya Chini

Au “likivunjwa.”
Au “makao haya.”
Au “kuvaa makao yetu.”
Au “makao yetu ya mbinguni.”
Au “malipo ya awali; uthibitisho (dhamana) wa kile kitakachokuja.”
Au “tufunuliwe.”
Au “maovu.”
Au “tumefunuliwa.”
Au “tumefunuliwa.”
Au “dhabihu ya dhambi.”