Isaya 26:1-21

  • Wimbo kuhusu tumaini na wokovu (1-21)

    • Yah Yehova, Mwamba wa milele (4)

    • Watu duniani watajifunza uadilifu (9)

    • “Wafu wako wataishi” (19)

    • Ingieni katika vyumba vya ndani mjifiche (20)

26  Siku hiyo wimbo huu utaimbwa+ katika nchi ya Yuda:+ “Tuna jiji imara.+ Anaufanya wokovu uwe kuta zake na maboma yake.+   Fungueni malango+ ili taifa la uadilifu liingie,Taifa linalodumisha mwenendo wa uaminifu.   Utawalinda wale wanaokutegemea kikamili;*Utawapa amani inayodumu,+Kwa sababu wanakutumaini wewe.+   Mtumainini Yehova milele,+Kwa maana Yah* Yehova ni Mwamba wa milele.+   Kwa maana amewashusha chini wale wanaokaa juu, jiji lililoinuliwa. Analiangusha chini,Analiangusha chini duniani;Analitupa chini mavumbini.   Mguu utalikanyaga-kanyaga,Miguu ya wanaoteseka, nyayo za watu wa hali ya chini.”   Njia ya mwadilifu imenyooka.* Kwa sababu wewe ni mnyoofu,Utailainisha njia ya mwadilifu.   Tunapofuata njia ya hukumu zako, Ee Yehova,Tumaini letu liko kwako. Tunatamani* sana jina lako na ukumbusho wako.*   Usiku ninakutamani sana kwa nafsi yangu yote,Naam, roho yangu inaendelea kukutafuta;+Kwa maana hukumu zinapotoka kwako kwa ajili ya dunia,Wakaaji wa nchi hujifunza kuhusu uadilifu.+ 10  Hata mwovu akionyeshwa kibali,Hatajifunza uadilifu.+ Hata katika nchi ya unyoofu, atatenda uovu,+Naye hatauona ukuu wa Yehova.+ 11  Ee Yehova, mkono wako umeinuliwa, lakini hawauoni.+ Wataona bidii yako kwa ajili ya watu wako na kuaibishwa. Naam, moto uliokusudiwa maadui wako utawateketeza. 12  Ee Yehova, utatupatia amani,+Kwa sababu kila kitu ambacho tumefanyaNi wewe uliyetutimizia. 13  Ee Yehova Mungu wetu, mabwana wengine mbali na wewe wametutawala,+Lakini tunalitaja jina lako peke yake.+ 14  Wamekufa; hawataishi. Hawana uwezo katika kifo, hawataamka.+ Kwa maana umewaelekezea fikiraIli uwaangamize na kufutilia mbali kabisa majina yao. 15  Umeongeza ukubwa wa taifa, Ee Yehova,Umeongeza ukubwa wa taifa;Umejitukuza mwenyewe.+ Umepanua sana mipaka yote ya nchi.+ 16  Ee Yehova, wakati wa taabu walikutafuta;Walikumwagia sala yao kwa kunong’ona ulipowatia nidhamu.+ 17  Kama vile mwanamke mwenye mimba aliye karibu kuzaaAnavyopata maumivu na kulia kwa uchungu,Ndivyo hali yetu ilivyo kwa sababu yako, Ee Yehova. 18  Tulipata mimba, tulikuwa na maumivu ya kuzaa,Lakini ni kama tumezaa upepo. Hatujaleta wokovu nchini,Na hakuna mtu aliyezaliwa ili aishi nchini. 19  “Wafu wako wataishi. Maiti zangu zitaamka.*+ Amkeni na mpige vigelegele kwa shangwe,Enyi mnaokaa mavumbini!+ Kwa maana umande wako ni kama umande wa asubuhi,*Na dunia itawaacha wale waliokufa ambao hawana uwezo wawe hai tena.* 20  Nendeni, watu wangu, ingieni katika vyumba vyenu vya ndani,Na mfunge milango nyuma yenu.+ Jificheni kwa muda mfupiMpaka ghadhabu* itakapopita.+ 21  Kwa maana tazama! Yehova anakuja kutoka mahali pakeIli kuwaita wakaaji wa nchi wawajibike kwa sababu ya uovu wao,Na nchi itafunua umwagaji wake wa damuNayo haitawafunika tena watu wake waliouawa.”

Maelezo ya Chini

Au labda, “wale ambao mwelekeo wao hautikisiki.”
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “ni tambarare.”
Au “Kwa nafsi zetu tunatamani.”
Yaani, kwamba Mungu na jina lake likumbukwe, litangazwe.
Tnn., “Maiti yangu itaamka.”
Au labda, “umande wa mimea (miholi).”
Au “itawazaa wale waliokufa ambao hawana uwezo.”
Au “shutuma.”