Kwa Wafilipi 4:1-23

  • Umoja, kushangilia, mawazo yanayofaa (1-9)

    • Msihangaike kuhusu jambo lolote (6, 7)

  • Paulo awashukuru Wafilipi kwa zawadi (10-20)

  • Salamu za mwisho (21-23)

4  Kwa hiyo, ndugu zangu ninaowapenda na ninaotamani kuwaona, shangwe yangu na taji langu,+ simameni imara+ kwa njia hii katika Bwana, wapendwa wangu.  Ninawahimiza Euodia na Sintike wawe na akili moja katika Bwana.+  Ndiyo, ninakuomba pia, ukiwa mfanyakazi mwenzangu wa kweli,* uendelee kuwasaidia wanawake hao ambao wamejitahidi* sana pamoja nami kwa ajili ya habari njema, pamoja na Klementi na vilevile wale wafanyakazi wenzangu wengine, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima.+  Shangilieni sikuzote katika Bwana. Nitasema tena, Shangilieni!+  Usawaziko wenu+ na ujulikane kwa watu wote. Bwana yuko karibu.  Msihangaike kuhusiana na jambo lolote,+ bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani, mjulisheni Mungu maombi yenu;+  na amani+ ya Mungu inayozidi uelewaji wote itailinda mioyo yenu+ na nguvu zenu za akili* kupitia Kristo Yesu.  Mwishowe, akina ndugu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, mambo yoyote yaliyo ya hangaiko zito, mambo yoyote yaliyo ya uadilifu, mambo yoyote yaliyo safi kiadili, mambo yoyote yanayopendeka, mambo yoyote yanayosemwa vema, mambo yoyote ya wema wa adili, na mambo yoyote yanayostahili sifa, endeleeni kuyafikiria* mambo hayo.+  Mambo mliyojifunza na vilevile mkayakubali na kuyasikia na kuyaona kuhusiana nami, mzoee kuyafanya hayo,+ na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi. 10  Ninashangilia sana katika Bwana kwamba sasa mwishowe mmeanza tena kunihangaikia.+ Ingawa mlinihangaikia, hamkupata nafasi ya kuonyesha jambo hilo. 11  Sisemi hivyo kwa sababu nina uhitaji, kwa maana hata hali zangu ziweje nimejifunza kuridhika.*+ 12  Ninajua jinsi ya kupungukiwa na chakula,+ na jinsi ya kuwa na vitu vingi. Katika mambo yote na katika hali zote nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba na pia jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na pia jinsi ya kuishi bila kitu. 13  Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yule anayenipa nguvu.+ 14  Hata hivyo, mlifanya vema kwa kushiriki pamoja nami katika dhiki yangu. 15  Kwa kweli, ninyi Wafilipi pia mnajua kwamba mwanzoni mlipojifunza habari njema, nilipoondoka Makedonia, hakuna kutaniko lililoshiriki pamoja nami katika kutoa na kupokea, isipokuwa ninyi peke yenu;+ 16  kwa maana nilipokuwa Thesalonike, mlinitumia kitu kwa ajili ya uhitaji wangu si mara moja tu bali mara mbili. 17  Si kwamba ninatafuta zawadi, bali ninataka tunda linalowaletea faida zaidi kwenye akiba yenu. 18  Hata hivyo, nina kila kitu ninachohitaji, na hata zaidi. Nimejaziwa kila kitu, kwa kuwa sasa nimepokea kutoka kwa Epafrodito+ vitu mlivyotuma, harufu tamu,+ dhabihu yenye kukubalika, inayompendeza Mungu vema. 19  Naye Mungu wangu atawajazia kikamili uhitaji wenu+ kulingana na utajiri wake katika utukufu kupitia Kristo Yesu. 20  Sasa kwa Mungu na Baba yetu kuwe na utukufu milele na milele. Amina. 21  Mpeni kila mtakatifu salamu zangu katika muungano na Kristo Yesu. Ndugu walio pamoja nami wanawatumia salamu zao. 22  Watakatifu wote, lakini hasa wale wa nyumbani mwa Kaisari,+ wanawatumia salamu zao. 23  Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo ziwe pamoja na roho mnayoonyesha.

Maelezo ya Chini

Tnn., “mwenzangu kihalisi katika nira.”
Au “wamepambana.”
Au “akili zenu; mawazo yenu.”
Au “kuyatafakari.”
Au “kutosheka.”