Zaburi 103:1-22

  • “Nafsi yangu na imsifu Yehova”

    • Mungu huweka dhambi zetu mbali sana (12)

    • Mungu huonyesha rehema kama baba (13)

    • Mungu hukumbuka kwamba sisi ni mavumbi (14)

    • Kiti cha ufalme cha Yehova na ufalme wake (19)

    • Malaika hutekeleza neno la Mungu (20)

Wa Daudi. 103  Nafsi yangu na imsifu Yehova;Kila kitu kilicho ndani yangu na kilisifu jina lake takatifu.   Nafsi yangu na imsifu Yehova;Nami nisisahau kamwe mambo yote aliyotenda.+   Husamehe makosa yako yote+Na kuyaponya magonjwa yako yote;+   Huukomboa uhai wako kutoka shimoni*+Na kukuvika taji la upendo wake mshikamanifu na rehema.+   Hukushibisha kwa vitu vyema+ maisha yako yote,Hivi kwamba ujana wako unarudishwa upya kama ule wa tai.+   Yehova hutenda kwa uadilifu+ na hakiKwa ajili ya wote wanaokandamizwa.+   Alimjulisha Musa njia zake,+Na wana wa Israeli matendo yake.+   Yehova ni mwenye rehema na mwenye huruma,*+Si mwepesi wa hasira naye ana upendo mwingi mshikamanifu.*+   Hatatafuta makosa sikuzote,+Wala hataendelea kuwa na hasira milele.+ 10  Hajatutendea kulingana na dhambi zetu,+Wala hajatupa adhabu tuliyostahili kulingana na makosa yetu.+ 11  Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,Ndivyo upendo wake mshikamanifu ulivyo mkubwa kuelekea wale wanaomwogopa.+ 12  Kama mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali sana na sisi.+ 13  Kama baba anavyowaonyesha wanawe rehema,Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+ 14  Kwa maana anajua vema umbo letu,+Akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.+ 15  Siku za mwanadamu anayeweza kufa ni kama za majani;+Yeye huchanua kama ua la shambani.+ 16  Lakini upepo unapovuma, linatoweka,Kana kwamba halikuwahi kuwepo.* 17  Lakini upendo mshikamanifu wa Yehova ni wa milele na milele*Kuelekea wale wanaomwogopa,+Na uadilifu wake kuelekea watoto wa watoto wao,+ 18  Kuelekea wale wanaolishika agano lake+Na wale walio waangalifu ili kuyashika maagizo yake. 19  Yehova amekiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme mbinguni;+Nao ufalme wake unatawala kila kitu.+ 20  Msifuni Yehova, enyi malaika wake wote,+ mlio na nguvu nyingi,Mnaotekeleza neno lake,+ mkitii sauti yake.* 21  Msifuni Yehova, enyi majeshi yake yote,+Ninyi wahudumu wake mnaofanya mapenzi yake.+ 22  Msifuni Yehova, kazi zake zote,Kila mahali anapotawala.* Nafsi yangu yote na imsifu Yehova.

Maelezo ya Chini

Au “kaburini.”
Au “neema.”
Au “fadhili nyingi zenye upendo.”
Tnn., “Na mahali pake hapalijui tena.”
Au “tangu milele hadi milele.”
Tnn., “mkiisikia sauti ya neno lake.”
Au “Kila mahali pa enzi yake kuu.”