Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Njia Tatu za Kumtegemea Yehova

Njia Tatu za Kumtegemea Yehova

Daudi alimshinda Goliathi kwa sababu alimtegemea Yehova. (1Sa 17:45) Yehova anataka kudhihirisha nguvu zake kwa niaba ya watumishi wake wote. (2Nya 16:9) Tunaweza kutegemeaje msaada ambao Yehova anatoa badala ya kutegemea uzoefu na uwezo wetu wenyewe? Zifuatazo ni njia tatu:

  • Sali mara nyingi. Usisali tu ili usamehewe baada ya kufanya kosa, bali pia sali upate nguvu unapokabili jaribu. (Mt 6:12, 13) Usisali tu kwamba Yehova abariki maamuzi ambayo tayari umefanya, bali pia sali upate mwongozo na hekima kabla ya kufanya maamuzi.—Yak 1:5

  • Uwe na ratiba ya kusoma na kujifunza Biblia. Soma Biblia kila siku. (Zb 1:2) Tafakari mifano ya Biblia, na utumie mambo uliyojifunza. (Yak 1:23-25) Jitayarishe kwa ajili ya huduma badala ya kutegemea uzoefu wako. Jifunze mapema habari itakayozungumziwa katika mikutano ya kutaniko ili unufaike kikamili

  • Shirikiana na tengenezo la Yehova. Jifahamishe na miongozo ya karibuni zaidi ya tengenezo, kisha utende haraka kupatana nayo. (Hes 9:17) Wasikilize wazee wanapotoa mashauri na maagizo.​—Ebr 13:17.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA HATUHITAJI KUOGOPA MATESO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

• Ni mambo gani yenye kuogopesha ambayo ndugu na dada walikabili?

• Ni nini kilichowasaidia kushinda woga wao?