Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

BORESHA HUDUMA YAKO | ONGEZA SHANGWE YAKO KATIKA HUDUMA

Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Washinde Mazoea Machafu

Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Washinde Mazoea Machafu

Ni wale tu ambao ni safi kiadili wanaoweza kuwa na uhusiano wa karibu na Yehova. (1Pe 1:14-16) Wanafunzi wa Biblia wanaposhinda mazoea mabaya, huenda pia wakapata manufaa katika familia, ya kiafya, na ya kiuchumi.

Waeleze waziwazi viwango vya maadili vya Yehova ni vipi, kwa nini vimewekwa, na manufaa ya kuvifuata. Kazia fikiria kuwasaidia wanafunzi wako kubadili njia yao ya kufikiri, na bila shaka matendo yatafuata. (Efe 4:22-24) Wahakikishie kwamba kwa msaada wa Yehova wanaweza kushinda zoea baya lililokita mizizi. (Flp 4:13) Wafundishe kutoa dua kwa Yehova wanapopata tamaa ya kutenda dhambi. Wasaidie kutambua hali wanazopaswa kuepuka zinazoweza kutokeza kishawishi cha kutenda dhambi. Badala ya mazoea machafu watie moyo wajihusishe katika utendaji utakaowanufaisha. Utapata shangwe kuwaona wanafunzi wa Biblia wakifanikiwa kufanya mabadiliko kwa msaada wa Yehova.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA WASAIDIE WANAFUNZI WAKO WA BIBLIA WASHINDE MAZOEA MACHAFU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Wazee na Neema walimwonyeshaje Lulu kwamba wana uhakika naye?

  • Neema alimpa Lulu msaada gani wa ziada?

  • Lulu alitafutaje msaada wa Yehova?