Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Uchunguzi Muhimu Zaidi Unaoweza Kufanya

Uchunguzi Muhimu Zaidi Unaoweza Kufanya

JE, WEWE ni Mkristo? Ikiwa ndivyo, wewe ni miongoni mwa watu zaidi ya bilioni mbili duniani pote wanaodai kuwa wafuasi wa Kristo. Leo, kuna maelfu ya dini zinazodai kuwa za Kikristo, hata hivyo, maoni na mafundisho yao yanatofautiana. Hivyo, mambo unayoamini yanaweza kutofautiana na ya Wakristo wengine. Je, ni muhimu kuchunguza yale unayoamini? Ndiyo, ni muhimu, ikiwa unataka kufuata mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu Ukristo.

Wafuasi wa Yesu Kristo wa mapema walijulikana kuwa “Wakristo.” (Matendo 11:26) Hakukuwa na haja ya kutumia majina mengine ili kuwatambulisha, kwa kuwa kulikuwa na imani moja tu ya Kikristo. Wakristo hao wenye umoja walifuata mafundisho na maagizo ya Yesu Kristo, Mwanzilishi wa Ukristo. Namna gani dini yako? Je, unaamini kwamba dini yako inafuata yale ambayo Kristo alifundisha, na yale ambayo wafuasi wa mapema wa Kristo waliamini? Unawezaje kujua mambo hayo? Kuna njia moja tu, nayo ni kuitumia Biblia kuwa kifaa cha kufanyia uchunguzi.

Fikiria jambo hili: Yesu Kristo aliheshimu sana Maandiko kwa sababu ni Neno la Mungu. Aliwapinga wale waliopuuza mafundisho ya Biblia na kufuata mapokeo ya wanadamu. (Marko 7:9-13) Hivyo, tunaweza kufikia mkataa kwamba imani ya wafuasi wa kweli wa Yesu inapaswa kutegemea Biblia. Kwa hiyo kila Mkristo anahitaji kujiuliza hivi, ‘Je, mafundisho ya dini yangu yanapatana na Biblia?’ Ili kujibu swali hilo, inafaa kulinganisha mafundisho ya dini yako na mambo ambayo Biblia inafundisha.

Yesu alisema kwamba ibada yetu kwa Mungu inapaswa kutegemea kweli, na kweli hiyo inapatikana katika Biblia. (Yohana 4:24; 17:17) Mtume Paulo alisema kwamba wokovu wetu hutegemea kupata “ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Timotheo 2:4) Kwa hiyo, ni muhimu imani yetu itegemee ujuzi sahihi wa Biblia. Wokovu wetu unategemea jambo hilo!

JINSI YA KULINGANISHA MAMBO TUNAYOAMINI NA MAFUNDISHO YA BIBLIA

Tunakualika usome maswali sita yafuatayo na uchunguze majibu ya Biblia kwa maswali hayo. Soma mistari ya Biblia iliyoonyeshwa, na utafakari majibu yake. Kisha jiulize hivi, ‘Je, mafundisho ya dini yangu yanapata na mafundisho ya Biblia?’

Maswali haya machache yanaweza kukusaidia kufanya uchunguzi muhimu zaidi maishani. Je, ungependa kulinganisha mafundisho mengine ya dini yako na mafundisho ya Biblia? Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia kuchunguza kweli za Biblia. Wasiliana na Mashahidi ili kujifunza Biblia bila malipo! Au tembelea tovuti yetu, jw.org/sw.