Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 15:1-58

  • Ufufuo wa Kristo (1-11)

  • Ufufuo, msingi wa imani (12-19)

  • Ufufuo wa Kristo unatoa uhakikisho (20-34)

  • Mwili wa nyama, mwili wa kiroho (35-49)

  • Kutoweza kufa na kutoweza kuharibika (50-57)

  • Kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana (58)

15  Basi akina ndugu, ninawakumbusha kuhusu habari njema niliyowatangazia,+ nanyi mkaipokea pia, na mmechukua msimamo kwa ajili yake.  Kupitia hiyo ninyi pia mnaokolewa ikiwa mtaishika sana habari njema niliyowatangazia, isipokuwa iwe mlikuwa waamini bila kusudi.  Kwa maana kati ya mambo ya kwanza niliyowapa ni yale niliyopokea pia, kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kulingana na Maandiko;+  na kwamba alizikwa,+ ndiyo, kwamba alifufuliwa+ siku ya tatu+ kulingana na Maandiko;+  na kwamba alimtokea Kefa,*+ kisha wale 12.+  Baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya 500 kwa wakati mmoja,+ na wengi kati yao bado tuko nao, ingawa wengine wamelala usingizi katika kifo.  Baadaye alimtokea Yakobo,+ kisha mitume wote.+  Lakini mwisho kabisa alinitokea mimi pia+ kana kwamba kwa yule aliyezaliwa kabla ya wakati wake.  Kwa maana mimi ni mdogo zaidi kati ya mitume, nami sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kutaniko la Mungu.+ 10  Lakini kwa fadhili zisizostahiliwa za Mungu mimi niko kama nilivyo. Na fadhili zake zisizostahiliwa kwangu hazikuwa za bure, bali nilifanya kazi zaidi yao wote; lakini si mimi bali ni fadhili zisizostahiliwa za Mungu zilizo pamoja nami. 11  Iwe ni mimi au ni wao, hivi ndivyo tunavyohubiri, na hivyo ndivyo mlivyoamini. 12  Basi ikiwa inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ kwa nini wengine kati yenu wanasema hakuna ufufuo wa wafu? 13  Kwa kweli, ikiwa hakuna ufufuo wa wafu, basi Kristo hakufufuliwa. 14  Lakini ikiwa Kristo hakufufuliwa, hakika kuhubiri kwetu ni bure, na imani yenu pia ni bure. 15  Isitoshe, tunaonekana pia kuwa mashahidi wa uwongo wa Mungu,+ kwa sababu tumetoa ushahidi dhidi ya Mungu kwa kusema kwamba alimfufua Kristo,+ ambaye hakumfufua ikiwa kwa kweli wafu hawatafufuliwa. 16  Kwa maana ikiwa wafu hawatafufuliwa, basi Kristo hakufufuliwa. 17  Isitoshe, ikiwa Kristo hakufufuliwa, imani yenu ni bure; nanyi mnabaki katika dhambi zenu.+ 18  Basi pia, wale ambao wamelala usingizi katika kifo wakiwa katika muungano na Kristo wameangamia.+ 19  Ikiwa ni katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi ndio wa kusikitikiwa kuliko mtu yeyote. 20  Lakini sasa Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, akiwa matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.+ 21  Kwa kuwa kifo kilikuja kupitia mwanadamu,+ ufufuo wa wafu pia unakuja kupitia mwanadamu.+ 22  Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa,+ vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.+ 23  Lakini kila mmoja kwa mpangilio wake unaofaa: Kristo aliye matunda ya kwanza,+ baadaye wale walio wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.+ 24  Kisha, mwisho, atakapoukabidhi Ufalme kwa Mungu wake aliye Baba yake, atakapokuwa ameangamiza serikali yote na mamlaka yote na nguvu zote.+ 25  Kwa maana lazima atawale akiwa mfalme mpaka Mungu atakapoweka maadui wote chini ya miguu yake.+ 26  Na adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.+ 27  Kwa maana Mungu “alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.”+ Lakini anaposema ‘vitu vyote vimetiishwa,’+ ni wazi kwamba hilo halimhusu Yule aliyevitiisha vitu vyote chini yake.+ 28  Lakini vitu vyote vitakapotiishwa kwake, ndipo Mwana mwenyewe atakapojitiisha pia kwa Yule aliyevitiisha vitu vyote kwake,+ ili Mungu awe vitu vyote kwa kila mtu.+ 29  Kama sivyo, watafanya nini wale wanaobatizwa kwa kusudi la kuwa wafu?+ Ikiwa wafu hawatafufuliwa kamwe, kwa nini basi wanabatizwa kwa kusudi la kuwa hivyo? 30  Kwa nini sisi pia tumo hatarini kila saa?*+ 31  Ninakabili kifo kila siku. Hili ni hakika kama ilivyo furaha yangu kwenu, akina ndugu, niliyo nayo katika Kristo Yesu Bwana wetu. 32  Ikiwa kama watu wengine,* nimepigana na wanyama wa mwituni huko Efeso,+ hilo lina faida gani kwangu? Ikiwa wafu hawatafufuliwa, “acheni tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.”+ 33  Msipotoshwe. Kushirikiana na watu wabaya huharibu tabia nzuri.*+ 34  Amkeni kwa njia ya uadilifu na msiwe na mazoea ya kufanya dhambi, kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninasema ili kuwafanya mwone aibu. 35  Hata hivyo, mtu fulani atauliza: “Wafu watafufuliwaje? Ndiyo, watakuja wakiwa na mwili wa aina gani?”+ 36  Wewe mtu usiye na akili! Kile unachopanda hakiwi hai isipokuwa kwanza kife. 37  Na kuhusu kile unachopanda, unapanda, si mwili utakaochipuka, bali ni mbegu tu, iwe ya ngano au mbegu ya aina nyingine; 38  lakini Mungu huipa mwili kama anavyopenda na huipa kila mbegu mwili wake. 39  Nyama zote si za aina moja, bali kuna ya wanadamu, kuna nyama ya mifugo, kuna nyama ya ndege, na nyingine ya samaki. 40  Na kuna miili ya mbinguni+ na miili ya duniani;+ lakini utukufu wa miili ya mbinguni ni wa namna moja, na ule wa miili ya duniani ni wa namna nyingine. 41  Utukufu wa jua ni wa namna moja, na utukufu wa mwezi ni mwingine,+ na utukufu wa nyota ni mwingine; kwa kweli, nyota moja hutofautiana na nyota nyingine kwa utukufu. 42  Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutoweza kuharibika.+ 43  Hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika utukufu.+ Hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu.+ 44  Hupandwa ukiwa mwili wa nyama; hufufuliwa ukiwa mwili wa roho. Ikiwa kuna mwili wa nyama, basi kuna mwili wa roho pia. 45  Basi imeandikwa hivi: “Mwanadamu wa kwanza Adamu akawa mtu aliye hai.”*+ Adamu wa mwisho akawa roho inayowapa watu uhai.+ 46  Hata hivyo, ule wa roho si wa kwanza. Ule wa nyama ndio wa kwanza, na baadaye ule wa roho. 47  Mtu wa kwanza ni wa kutoka duniani na ameumbwa kwa mavumbi;+ mtu wa pili ni wa kutoka mbinguni.+ 48  Kama yule aliyeumbwa kwa mavumbi, ndivyo walivyo pia wale walioumbwa kwa mavumbi; na kama alivyo yule wa mbinguni, ndivyo walivyo pia wale wa mbinguni.+ 49  Na kama vile ambavyo tumeuchukua mfano wa yule aliyeumbwa kwa mavumbi,+ vivyo hivyo pia tutauchukua mfano wa yule wa mbinguni.+ 50  Lakini ninawaambia hivi, akina ndugu, kwamba nyama na damu haviwezi kuurithi Ufalme wa Mungu, wala uharibifu haurithi kutoweza kuharibika. 51  Tazama! Ninawaambia siri takatifu: Hatutalala usingizi katika kifo sisi sote, bali sote tutabadilishwa,+ 52  kwa muda mfupi, kufumba na kufumbua* jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho. Kwa maana tarumbeta italia,+ na wafu watafufuliwa wakiwa wasioweza kuharibika, nasi tutabadilishwa. 53  Kwa maana huu ulio wa kuharibika lazima uvae kutoweza kuharibika,+ na huu unaoweza kufa lazima uvae kutoweza kufa.+ 54  Lakini huu unaoweza kuharibika utakapovaa kutoweza kuharibika na huu unaoweza kufa utakapovaa kutoweza kufa, ndipo neno hili lililoandikwa litakapotimia: “Kifo kimemezwa milele.”+ 55  “Kifo, uko wapi ushindi wako? Kifo, uko wapi mchomo wako?”+ 56  Mchomo unaotokeza kifo ni dhambi,+ nazo nguvu za dhambi ni Sheria.*+ 57  Lakini tunamshukuru Mungu, kwa maana yeye hutupatia ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo!+ 58  Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa, iweni imara,+ thabiti, sikuzote mkiwa na mengi ya kufanya+ katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi yenu si ya bure+ kuhusiana na Bwana.

Maelezo ya Chini

Pia anaitwa Petro.
Au “wakati wote.”
Au labda, “kwa maoni ya kibinadamu.”
Au “hupotosha maadili.”
Au “nafsi iliyo hai.”
Au “kupepesa.”
Au “nayo Sheria huipa dhambi nguvu zake.”