Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Je, dhambi zetu zinaweza kusamehewa?

Unaweza kupata kibali cha Mungu

Kulingana na Biblia, wanadamu wote ni wenye dhambi. Tulirithi dhambi kutoka kwa mtu wa kwanza, Adamu. Kwa hiyo, nyakati nyingine sisi hufanya mambo mabaya na baadaye tunajutia matendo hayo. Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, alikufa ili kulipia dhambi zetu. Kupitia dhabihu yake ya fidia tunaweza kusamehewa. Ni zawadi kutoka kwa Mungu.—Soma Waroma 3:23, 24.

Baadhi ya watu wamefanya dhambi nzito na huenda wakajiuliza kama Mungu anaweza kuwasamehe. Kwa kupendeza, Neno la Mungu linasema: “Damu ya Yesu Mwana wake hutusafisha kutoka katika dhambi yote.” (1 Yohana 1:7) Yehova yuko tayari kutusamehe hata dhambi nzito tukitubu kikweli.—Soma Isaya 1:18.

Tunapaswa kufanya nini ili tusamehewe?

Ikiwa tunataka Yehova Mungu atusamehe, tunahitaji kujifunza kumhusu—tuelewe njia zake, ushauri wake, na matakwa yake. (Yohana 17:3) Yehova huwasamehe wale wanaotubu makosa yao na kujitahidi kubadilika.—Soma Matendo 3:19.

Unaweza kupata kibali cha Mungu. Yehova anaelewa udhaifu wetu. Yeye ni mwenye rehema na fadhili. Je, fadhili zake zenye upendo hazikuchochei ujifunze mengi kuhusu jinsi unavyoweza kumpendeza?—Soma Zaburi 103:13, 14.