Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Wakati ujao wa wanadamu utakuwaje?

kifo cha Yesu kitawasaidia jinsi gani wanadamu kupendana wakati ujao?

Ni kweli kwamba wanadamu watazidi kufanya maendeleo ya kisayansi. Hata hivyo, je, wataweza kuwasaidia wanadamu wenzao wapendane kikweli? Hapana. Leo, ulimwengu umejaa pupa na ubinafsi. Hata hivyo, Mungu ana kusudi zuri kwa wanadamu.—Soma 2 Petro 3:13.

Neno la Mungu linatoa ahadi kuhusu ulimwengu ambao wanadamu watapendana. Watu wataishi kwa amani, na hakuna mtu atakayemsababishia mwingine madhara.—Soma Mika 4:3, 4.

Roho ya ubinafsi itaondolewaje?

Mungu aliumba mwanadamu asiye na ubinafsi. Hata hivyo, mwanadamu wa kwanza alipoteza ukamilifu alipokosa kumtii Mungu. Sote tumerithi roho ya ubinafsi kutoka kwake. Pamoja na hayo, Mungu atamtumia Yesu kuwarudishia wanadamu ukamilifu.—Soma Waroma 7:21, 24, 25.

Kulingana na kusudi la Mungu, Yesu alikufa kifo cha kidhabihu na kufuta madhara yote yaliyotokana na kutotii kwa mwanadamu wa kwanza. (Waroma 5:19) Hivyo, Yesu amewawezesha wanadamu kuwa na tumaini la wakati ujao ambapo hawatakuwa na roho ya ubinafsi inayowafanya watende dhambi.—Soma Zaburi 37:9-11.