Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA KUULIZA MAULIZO | FAN YU

Mutengenezaji wa Programu za Ordinatere Anafasiria Imani Yake

Mutengenezaji wa Programu za Ordinatere Anafasiria Imani Yake

FAN YU alianza kazi yake akiwa mwanasayansi mwenye kufanya utafiti kuhusu elimu ya hesabu katika Masomo ya Juu ya Nguvu ya Atomu ya inchi ya China, karibu na Beijing. Wakati huo, hakuamini kama Mungu iko na aliamini fundisho la mageuzi. Lakini, leo Yu anaamini kwamba uzima uliumbwa na Mungu. Amuka! ilimuuliza kuhusu imani yake.

Tafazali, utuambie namna ulikomaa.

Nilizaliwa katika mwaka wa 1959 katika muji wa Fuzhou, Jimbo la Jiangxi, katika inchi ya China. Wakati nilikuwa na miaka munane, inchi ilikuwa inapata matokeo ya ile yenye kuitwa leo Upinduzi wa Kidesturi. Baba yangu, ambaye alikuwa fundi wa ujenzi, aliombwa kujenga njia ya treni (train) katika eneo la jangwa lenye kuwa mbali. Kwa miaka mingi alikuwa anatutembelea mara moja tu kwa mwaka. Wakati huo niliishi na mama yangu, mwenye alikuwa mwalimu kwenye masomo ya musingi. Tuliishi katika masomo kwenye alikuwa anafundisha. Katika mwaka wa 1970, tulihamia katika muji mudogo wa Liufang, wenye ulikuwa maskini wakati huo. Muji huo uko katika Wilaya ya Linchuan, ambamo ilikuwa nguvu kupata chakula.

Familia yenu iliamini nini?

Baba yangu hakupendezwa na mambo ya dini wala ya politike. Mama yangu alikuwa Mubuda. Kwenye masomo, nilifundishwa kwamba uzima ulitokana na mageuzi kupitia njia ya asili, na niliamini mambo yenye walimu wangu walisema.

Sababu gani ulipendezwa na hesabu?

Nilipendezwa na hesabu kwa sababu inaomba mutu atafute kweli kupitia njia yenye kusadikisha. Nilienda kwenye masomo ya juu kisha tu kifo cha Mao Tse-tung, mukubwa wa mapinduzi, mwenye alikufa katika mwaka wa 1976. Nilichagua hesabu kuwa somo langu la musingi. Kisha kumaliza digrii ya pili, kazi yangu ya kwanza iliniomba nifanye utafiti kuhusu hesabu ili kutengeneza mitambo ya nyuklia.

Wakati ulipata habari kuhusu Biblia kwa mara ya kwanza, ulijisikia je?

Katika mwaka wa 1987, nilienda États-Unis ili kuendelea na masomo kwenye Masomo ya Juu ya Texas A&M. Nilijua kwamba katika Amerika watu wengi wanaamini kwamba Mungu iko na wanasoma Biblia. Nilisikia pia kwamba Biblia iko na mashauri yenye hekima, kwa hiyo, nilifikiri kwamba nilipaswa kuisoma.

Mafundisho ya Biblia yalionekana kuwa yenye kupatana na akili. Lakini niliona kwamba sehemu fulani zilikuwa nguvu kuelewa na bila kukawia nikaacha kuisoma.

Namna gani ulifikia kupenda tena Biblia?

Wazo la kwamba kuna Muumbaji lilikuwa mupya kwangu, kwa hiyo niliamua kufanya utafiti wangu mwenyewe kuhusu habari hiyo

Katika mwaka wa 1990, mwanamuke mumoja Shahidi wa Yehova alinitembelea na alinionyesha mambo yenye Biblia inasema kuhusu wakati muzuri wenye kuja wa wanadamu. Alikamata mupango ili watu fulani wawili wenye kuoana wakuje kunisaidia kuelewa Biblia. Kisha, bibi yangu, Liping, mwenye alikuwa mwalimu wa fizikia kwenye masomo ya segondere na ambaye hakuamini kama Mungu iko, alianza pia kujifunza Biblia. Tulijifunza jambo lenye Biblia inasema kuhusu chanzo cha uzima. Wazo la kwamba kuna Muumbaji lilikuwa mupya kwangu, kwa hiyo niliamua kufanya utafiti wangu mwenyewe kuhusu habari hiyo.

Namna gani ulifanya hivyo?

Kwa kuwa nilikuwa mwanasayansi wa hesabu, nilijua kufanya hesabu ya uwezekano wa matukio. Nilijifunza pia kwamba ili uzima ujitokeze wenyewe, iliomba kwanza kuwe protini. Kwa hiyo, nilijaribu kufanya hesabu ya uwezekano wa protini kujitokeza yenyewe. Protini ni kati ya molekuli zenye haiko mwepesi kuelewa, na chembe zenye kuishi zinaweza kuwa na maelfu ya aina mbalimbali ya protini zenye kuwa na uhusiano sahihi. Kama vile wengine, mimi pia nilitambua kwamba uwezekano wa protini kujitokeza yenyewe ni wa chini sana kabisa, ni kusema, haiwezekani kabisa protini ijitokeze yenyewe! Sijasoma jambo lolote katika fundisho la mageuzi lenye kunihakikishia kwamba molekuli hizo za ajabu sana zinaweza kujitokeza zenyewe kama zinakuwa inje ya kiumbe chenye uzima ambacho kina molekuli hizo. Kulingana na mimi, ukweli wa mambo unaonyesha kwamba kuna Muumbaji.

Ni nini ilikufanya usadiki kwamba Biblia ilitoka kwa Mungu?

Kadiri niliendelea kujifunza pamoja na Mashahidi wa Yehova, nilifikia kujua kwamba Biblia iko na unabii mwingi wenye umekwisha kutimia. Nilianza pia kujionea faida ya kutumikisha kanuni za Biblia. Nilijiuliza, ‘Namna gani waandikaji wa Biblia wenye waliishi kumepita miaka mingi waliandika maneno ya hekima ambayo yanaendelea kuwa na mafaa mupaka leo?’ Pole kwa pole, nilifikia kutambua kwamba Biblia ni Neno la Mungu.

Ni nini inaendelea kukufanya usadiki kwamba kuna Muumbaji?

Wakati ninafikiria sana vitu vyenye kutuzunguka, ninaamini kabisa kwamba kuna Muumbaji. Kwa sasa ninatengeneza programu za ordinatere, na kila mara nashangaa sana kuona namna ubongo uko na uwezo wa juu sana kuliko programu za ordinatere. Kwa mufano, uwezo wa ubongo wetu wa kutambua maneno ni wa ajabu sana. Wengi kati yetu wanaweza kuelewa kwa vyepesi maneno, hata musemwa wenye haumalizike, kicheko, kikohozi, kigugumizi, kutamka maneno, mwangwi (écho), makelele yenye kuwa pembeni, ao kuharibika kwa sauti kwenye telefone. Pengine unaweza kufikiri kwamba jambo hilo haliko la ajabu. Lakini watengenezaji wa programu za ordinatere wanaona jambo hilo kuwa la ajabu. Hata programu gani nzuri ya ordinatere ya kutambua maneno haifikie uwezo wa ubongo wa mwanadamu.

Tofauti na ordinatere zenye kuwa na uwezo wa hali ya juu sana, ubongo wetu uko na uwezo wa kutambua namna mutu anajisikia, namna anatamka maneno, na kutambua mutu fulani kupitia sauti yake. Watengenezaji wa programu za ordinatere wako wanajifunza namna ordinatere zinaweza kuiga uwezo wa ubongo wa mwanadamu wa kutambua maneno. Niko hakika kwamba wakati wanafanya hivyo wako wanajifunza kwa kweli kazi ya mikono ya Mungu.