Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA MALAIKA

Malaika

Malaika

Malaika wameonyeshwa katika vitabu, michoro, na filme. Lakini malaika ni nani, na wanatimiza daraka gani?

Malaika ni nani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

 

Mbele Mungu aumbe ulimwengu na wanadamu wa kwanza, alikuwa tayari ameumba viumbe wenye akili wa hali ya juu. Wako na nguvu ya juu kuliko wanadamu, na wanakaa katika makao moja na Mungu mwenyewe​—makao yenye hayawezi kufikiwa ao kuonwa na wanadamu. (Ayubu 38:4, 7) Biblia inaita viumbe hao wa hali ya juu “roho” ao “malaika.”​—Zaburi 104:4. *

Kuna hesabu ngapi ya malaika? Wengi sana. Malaika wenye kuzunguka kiti cha ufalme cha Mungu ni “makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu.” (Ufunuo 5:11) Kama tunakamata maneno hayo moja kwa moja, ni kusema, hesabu ya malaika ni mamia ya mamilioni!

“Nikaona . . . malaika wengi kuzunguka kile kiti cha ufalme  . . . , na hesabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu na maelfu ya maelfu.”​—Ufunuo 5:11.

Ni mambo gani malaika walifanya zamani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

 

Mara nyingi malaika walitumika kama wasemaji ao wajumbe wa Mungu. * Tena, wanaonyeshwa katika Biblia wakifanya miujiza ya Mungu. Mungu alituma malaika ili abariki Abrahamu na kumuzuia asitoe mutoto wake Isaka kuwa zabihu. (Mwanzo 22:11-18) Malaika alimutokea Musa katika muti wa miiba wenye kuwaka moto ili kumutolea ujumbe wenye kubadilisha maisha. (Kutoka 3:1, 2) Wakati nabii Danieli alitupwa katika shimo la simba, ‘Mungu [wake] mwenyewe alimutuma malaika wake na kufunga vinywa vya simba.’​—Danieli 6:22.

‘Ndipo malaika wa Yehova akamutokea [Musa] katika mwali wa moto katikati ya muti wa miiba.”​—Kutoka 3:2.

Ni mambo gani malaika wanafanya leo?

MAMBO BIBLIA INASEMA

 

Hatuwezi kujua mambo yote yenye malaika wanafanya leo. Lakini, Biblia inaonyesha kwamba wanahusika katika kusaidia watu wenye kuwa na moyo muzuri wafikie kujua mengi kuhusu Mungu.​—Matendo 8:26-35; 10:1-22; Ufunuo 14:6, 7.

Katika ndoto, Yehova alionyesha Yakobo malaika wenye kupanda na kushuka juu ya “ngazi” kati ya mbinguni na dunia. (Mwanzo 28:10-12) Inawezekana Yakobo alitambua kupitia ndoto hiyo jambo lenye tunaweza pia kutambua: Yehova Mungu anatuma malaika ili kutimiza mambo fulani, kutenda kwa ajili ya wanadamu washikamanifu ambao wako na lazima ya musaada wake.​—Mwanzo 24:40; Kutoka 14:19; Zaburi 34:7.

“Kulikuwa na ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na kilele chake kilikuwa kimefika mbinguni; na, tazama! malaika za Mungu walikuwa wakipanda na kushuka juu yake.”​—Mwanzo 28:12.

^ fu. 6 Biblia inaonyesha kwamba roho fulani waliasi mamlaka ya Mungu, na inawaita “roho waovu.”​—Luka 10:17-20.

^ fu. 11 Maneno ya zamani ya Kiebrania na Kigiriki yenye kutumiwa katika Biblia ambayo yanatafsiriwa “malaika” yote yanamaanisha “mujumbe.”