Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Mufano wa Yesu kuhusu ‘imbwa wadogo’ ulikuwa matusi?

Sanamu ndogo ya Wagiriki ao ya Waroma yenye kuonyesha mutoto mwenye kuwa na kitoto cha imbwa (ya mwaka kati ya 100 M.K.Y. mupaka 200 K.K.Y.)

Siku moja, wakati Yesu alikuwa inje ya mipaka ya Israeli katika jimbo la Roma la Siria, mwanamuke mumoja Mugiriki alimukaribia ili kumuomba musaada. Yesu alimujibu kwa kutumia mufano wenye ulitoa ulinganisho kati ya watu wenye hawako Wayahudi na ‘imbwa wadogo.’ Katika Sheria ya Musa, imbwa walionwa kuwa wanyama wenye hawako safi. (Mambo ya Walawi 11:27) Lakini, Yesu alipenda kutukana mwanamuke huyo Mugiriki na watu wenye hawako Wayahudi?

Hapana kabisa. Kama vile alifasiria wanafunzi wake, Yesu alipenda kuonyesha kama kusudi lake kubwa wakati huo lilikuwa kusaidia Wayahudi. Kwa hiyo, alifasiria mwanamuke huyo Mugiriki kwa kusema hivi: ‘Si sawa kuuchukua mukate wa watoto na kuwatupia imbwa wadogo.’ (Mathayo 15:21-26; Marko 7:26) Kwa Waroma na Wagiriki, mara nyingi imbwa alionwa kuwa nyama-kipenzi mwenye aliishi ndani ya nyumba ya mutu na mwenye watoto wangecheza naye. Kwa hiyo, maneno ‘imbwa wadogo’ yalipaswa kuleta wazo fulani lenye kupendeza. Mwanamuke huyo Mugiriki alikubaliana na maneno ya Yesu na akamujibu: ‘Ndiyo, Bwana; lakini kwa kweli hao imbwa wadogo hula sehemu ya makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza ya mabwana zao.’ Yesu alimupongeza kwa sababu ya imani yake na akaponyesha binti yake.​—Mathayo 15:27, 28.

Mutume Paulo alitoa shauri nzuri kwa kupendekeza safari ya bahari icheleweshwe?

Muchoro wa mashua kubwa ya mizigo (wa kipindi kati ya mwaka wa 1 na 100 K.K.Y.)

Mashua yenye ilipeleka Paulo Italia ilikuwa inapambana na magumu ya pepo zenye kuvuma kinyume. Wakati walitua, Paulo alishauri kwamba safari yenye ilibaki icheleweshwe. (Matendo 27:9-12) Kulikuwa sababu ya kutoa shauri hilo?

Zamani, waendeshaji wa mashua walijua muzuri kwamba kufanya safari katika bahari ya Mediterania wakati wa miezi ya baridi kali ilikuwa hatari. Kuanzia katikati ya Mwezi wa 11 mupaka katikati ya Mwezi wa 3, ilionwa kuwa hatari kufanya safari katika bahari. Lakini safari yenye Paulo alizungumuzia ilipaswa kufanywa katika Mwezi wa 9 ao Mwezi wa 10. Katika kitabu chake Epitome of Military Science, muandikaji mumoja Muroma, Végèce (wa kipindi kati ya mwaka wa 301 na 400 kisha kuzaliwa kwa Yesu) alifasiria hivi kuhusu safari ya bahari: “Miezi fulani inafaa, ingine inaleta mashaka, na yenye kubaki haiwezekane kabisa.” Végèce alisema kwamba ilikuwa salama kusafiri katika bahari kuanzia tarehe 27 Mwezi wa 5 mupaka tarehe 14 Mwezi wa 9, lakini kulikuwa mashaka, ao hatari kusafiri kuanzia tarehe 15 Mwezi wa 9 mupaka tarehe 11 Mwezi wa 11, na kuanzia tarehe 11 Mwezi wa 3 mupaka tarehe 26 Mwezi wa 5. Bila shaka, Paulo mwenye alizoea kusafiri katika bahari alijua muzuri hali hizo zote. Inawezekana kapteni na mwenye mashua walijua pia mambo hayo, lakini hawakutenda kulingana na shauri la Paulo. Mwisho wa safari ilikuwa kuvunjika kwa mashua.​—Matendo 27:13-44.