Hamia kwenye habari

Dhiki Kuu Ni Nini?

Dhiki Kuu Ni Nini?

Jibu la Biblia

 Dhiki kuu ni kipindi chenye taabu zaidi kitakachowapata wanadamu. Kulingana na unabii wa Biblia, dhiki hiyo itatukia wakati wa “siku za mwisho,” au “wakati wa mwisho.” (2 Timotheo 3:1; Danieli 12:4) Itakuwa “dhiki ya namna ambayo haijatukia tangu mwanzo wa uumbaji ambao Mungu aliumba mpaka wakati huo, na haitatukia tena.”​—Marko 13:19; Danieli 12:1; Mathayo 24:21, 22.

Matukio ya wakati wa ile dhiki kuu

Matukio baada ya ile dhiki kuu

  •   Kufungwa kwa Shetani na roho waovu. Biblia inaonyesha malaika atamtupa Shetani na roho waovu katika “abiso,” yaani, watakuwa katika hali ya kutotenda kama ya wafu. (Ufunuo 20:1-3) Hali ya Shetani akiwa ndani ya abiso inaweza kulinganishwa na kufungwa gerezani; hataweza kuathiri mambo yanayotendeka mahali pengine popote.​—Ufunuo 20:7.

  •   Kuanza kwa ile Miaka Elfu Moja. Ufalme wa Mungu utaanza utawala wake wa miaka 1,000, ambao utawaletea wanadamu baraka nyingi. (Ufunuo 5:9, 10; 20:4, 6) “Umati mkubwa” ambao hauwezi kuhesabiwa ‘utatoka katika ile dhiki kuu,’ ukiokoka na kuanza kuishi duniani wakati wa ile Miaka Elfu Moja.​—Ufunuo 7:9, 14; Zaburi 37:9-11.

a Katika kitabu cha Ufunuo, dini ya uwongo inafananishwa na Babiloni Mkubwa, “yule kahaba mkubwa.” (Ufunuo 17:1, 5) Mnyama-mwitu mwenye rangi nyekundu, ambaye anamwangamiza Babiloni Mkubwa, anawakilisha shirika ambalo kusudi lake ni kuunganisha na kutenda kwa niaba ya mataifa ya ulimwengu. Mwanzoni lilikuwa Ushirika wa Mataifa na sasa ni Umoja wa Mataifa.