Methali 16:1-33

  • Yehova huchunguza nia (2)

  • Mkabidhi Yehova kazi zako (3)

  • Mizani ya unyoofu hutoka kwa Yehova (11)

  • Kiburi hutangulia kuanguka kwa kishindo (18)

  • Mvi ni taji la umaridadi (31)

16  Mtu huyatayarisha mawazo ya moyo wake,*Lakini jibu analotoa* hutoka kwa Yehova.+   Njia zote za mwanadamu huonekana kuwa sawa* machoni pake,+Lakini Yehova huchunguza nia.*+   Mkabidhi Yehova lolote unalofanya,*+Na mipango yako itafanikiwa.   Yehova amefanya kila kitu kitimize kusudi lake,Hata waovu kwa ajili ya siku ya msiba.+   Kila mtu mwenye kiburi moyoni humchukiza Yehova.+ Uwe na hakika kwamba* hatakosa kuadhibiwa.   Kwa upendo mshikamanifu na uaminifu, kosa husamehewa,+Na kwa kumwogopa Yehova mtu hujiepusha na uovu.+   Yehova anapofurahia njia za mtu,Huwafanya hata maadui wake wawe na amani naye.+   Afadhali kuwa na kidogo pamoja na uadilifu+Kuliko kuwa na mapato mengi pasipo haki.+   Mtu anaweza kupanga njia yake moyoni mwake,Lakini Yehova ndiye anayezielekeza hatua zake.+ 10  Uamuzi ulioongozwa na roho* unapaswa kuwa katika midomo ya mfalme;+Hapaswi kamwe kusaliti haki.+ 11  Mizani na vipimo vya unyoofu hutoka kwa Yehova;Mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ni kazi yake.+ 12  Matendo maovu huwachukiza wafalme,+Kwa maana kiti cha ufalme huimarishwa kabisa kwa uadilifu.+ 13  Maneno ya uadilifu huwafurahisha wafalme. Wanampenda mtu anayeongea kwa unyoofu.+ 14  Ghadhabu ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo,+Lakini mtu mwenye hekima huituliza.*+ 15  Katika nuru ya uso wa mfalme kuna uzima;Kibali chake ni kama wingu la mvua wakati wa masika.+ 16  Jinsi lilivyo jambo bora kupata hekima kuliko dhahabu!+ Ni bora kuchagua uelewaji kuliko fedha.+ 17  Barabara kuu ya wanyoofu huepuka uovu. Yeyote anayelinda njia yake huhifadhi uhai wake.*+ 18  Kiburi hutangulia kuanguka kwa kishindo,Na roho ya majivuno hutangulia kujikwaa.+ 19  Ni afadhali kuwa mnyenyekevu*+ miongoni mwa wapoleKuliko kugawana nyara na watu wenye kiburi. 20  Mtu anayeonyesha ufahamu katika jambo atapata mafanikio,*Na mwenye furaha ni yule anayemtumaini Yehova. 21  Watu wenye hekima moyoni wataitwa watu wenye uelewaji,+Na mtu anayeongea kwa fadhili* huongeza ushawishi.+ 22  Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa walio nao,Lakini wajinga hutiwa nidhamu kwa ujinga wao wenyewe. 23  Moyo wa mwenye hekima hukipatia kinywa chake ufahamu+Na huongeza ushawishi kwenye maneno yake. 24  Maneno yanayopendeza ni sega la asali,Ni matamu kwa nafsi* nayo huponya mifupa.+ 25  Kuna njia inayoonekana kuwa sawa machoni pa mtu,Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+ 26  Hamu ya chakula* ya mfanyakazi humfanya afanye kazi kwa bidiiKwa sababu njaa yake* humchochea kuendelea kufanya kazi.+ 27  Mtu asiyefaa kitu huchimbua lililo ovu;+Na maneno yake ni kama moto unaounguza.+ 28  Mfanya fujo* husababisha mgawanyiko,+Na mchongezi huwatenganisha marafiki wa karibu.+ 29  Mtu mkatili humshawishi jirani yakeNa kumwongoza katika njia isiyofaa. 30  Hukonyeza jicho lake anapopanga njama zinazodhuru. Huibanabana midomo yake pamoja anapotekeleza hila. 31  Mvi ni taji la umaridadi*+Zinapopatikana katika njia ya uadilifu.+ 32  Mtu asiyekasirika upesi+ ni bora kuliko mwanamume mwenye nguvu,Na mtu anayedhibiti hasira yake* ni bora kuliko mtu anayelishinda jiji.+ 33  Kura hupigwa mapajani,+Lakini kila uamuzi unaofanywa kwa kura hiyo hutoka kwa Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “jibu linalofaa.” Tnn., “jibu la ulimi.”
Tnn., “Mipangilio ya moyo ni ya mtu.”
Tnn., “safi.”
Tnn., “huzichunguza roho.”
Tnn., “Mvingirishie Yehova kazi zako.”
Tnn., “Mkono kwa mkono.”
Au “Uamuzi ulioongozwa na Mungu.”
Au “huiepuka.”
Au “nafsi yake.”
Tnn., “na roho ya upole.”
Tnn., “mema.”
Au “Na maneno yanayovutia.” Tnn., “Na utamu wa midomo.”
Au “Yana ladha tamu.” Angalia Kamusi.
Au “Nafsi.”
Tnn., “mdomo wake.”
Au “Mpanga njama.”
Au “utukufu.”
Tnn., “anayetawala roho yake.”