Watu Wenye Umoja
Pakua:
1. Dhoruba inakuja.
Twaona ishara.
Upepo wa mateso
Hautatushangaza.
Kijasiri tutashinda,
Yehova yuko nasi.
Silaha yoyote ile
Hatutaiogopa.
(KORASI)
Tu watu wenye umoja,
Ulimwenguni pote.
Tuko imara pamoja,
Kwa nguvu za Yehova,
Kwa nguvu za Yehova.
2. Twamsubiri yeye
Tukiwa watulivu—
Ni Mungu wa wokovu
Atupenda sana.
Hataacha watu wake,
Anatuimarisha.
Adui hatatushinda.
Sisi ni wa Yehova!
(KORASI)
Tu watu wenye umoja,
Ulimwenguni pote.
Tuko imara pamoja,
Kwa nguvu za Yehova.
(DARAJA)
Sote twasimama;
Hatutahofu adui.
Pia kutoka moyoni
Twampenda Yehova.
(KORASI)
Tu watu wenye umoja,
Ulimwenguni pote.
Tuko imara pamoja,
Kwa nguvu za Yehova,
Kwa nguvu za Yehova.