Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Ahadi ya Paradiso Duniani Ilibadilisha Maisha Yangu!

Ahadi ya Paradiso Duniani Ilibadilisha Maisha Yangu!
  • ALIZALIWA MWAKA WA 1974

  • ALIZALIWA KATIKA INCHI YA LATVIA

  • ALIKUWA ANAFANYA MASHINDANO HATARI YA KUENDESHA PIKIPIKI

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

Nilizaliwa katika muji mukubwa wa inchi ya Latvia unaoitwa Riga. Mimi na dada yangu mukubwa tulikomalishwa na mama yetu. Hata ikiwa mama alikuwa mukatoliki, tulienda kwenye kanisa wakati tu wa sikukuu za kidini. Sikuzote niliamini kwamba kuna mutu aliye na uwezo mukubwa zaidi, lakini nilipokuwa kijana mudogo, nilikengeushwa akili na mambo mengine mengi.

Nilipokuwa ninakomaa, mama yangu aliona kwamba nilikuwa na uwezo wa kubomoa vitu na kuviunganisha tena. Kwa sababu mama alikuwa na vitu vingi nyumbani ambavyo vingeweza kubomolewa, alikuwa anaogopa kuniacha mimi mwenyewe nyumbani. Kwa hiyo, alininunulia vitu vya kuchezea, ambavyo nilikuwa ninabomoa na kuviunganisha tena. Nilipokuwa ninabomoa vitu na kuviunganisha tena, wakati huohuo nilikuwa pia na hamu sana ya kutembeza pikipiki. Mama yangu aliniandikisha katika kikundi cha mashindano ya kutembeza pikipiki, kikundi hicho kilikuwa kinaitwa Zelta Mopēds (Pikipiki ya Zahabu). Nilianza mashindano nikitumia pikipiki ndogo na kisha nilianza kutumia pikipiki kubwa.

Nilijifunza haraka sana kutembeza pikipiki na bila kukawia nikakuwa mutembezaji muzuri sana katika muchezo huo wa kutembeza pikipiki haraka uliokuwa hatari. Nilishinda mara tatu katika mashindano ya Latvia, na mara mbili katika mashindano ya inchi za Kibaltiki.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

Wakati nilifikia kuwa mutembezaji muzuri sana, Evija rafiki yangu mwanamuke (ambaye alikuja kuwa bibi yangu) alianza kuzungumuza na Mashahidi wa Yehova. Alikuwa amepata vitabu fulani, vilivyokuwa na sehemu ya kujaza ili kuomba funzo la Biblia. Alijaza sehemu hiyo na akaituma. Bila kukawia, Mashahidi wawili wa Yehova walimutembelea, na akaanza kujifunza Biblia pamoja nao. Nilifurahia pia funzo la Biblia, lakini wakati huo, sikuwa ninapendezwa na mambo ya dini.

Kisha hapo, Mashahidi wa Yehova walinialika kwenye funzo la Biblia la Evija ili nisikilize. Nilikubali, na nilifurahia mambo niliyosikia. Habari moja iliyonigusa moyo sana ilikuwa ahadi ya Biblia ya paradiso duniani. Kwa mufano, walinionyesha andiko la Zaburi 37:10, 11, linalosema hivi: ‘Na bado muda kidogo tu, na mutu muovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo. Bali wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.’ Ahadi hiyo ilinifurahisha kabisa.

Niliendelea kupendezwa na mambo niliyokuwa ninajifunza juu ya Mungu. Nilianza kutambua namna dini zinafundisha uongo sana. Tofauti na mafundisho ya dini, mafundisho ya Biblia yalinipendeza sana kwa sababu yalikuwa wazi na yenye kueleweka.

Nilipoendelea kujifunza Biblia, nilijua kwamba Yehova anaona uzima kuwa wa maana sana. (Zaburi 36:9) Kujua jambo hilo kulinifanya nifikirie sana muchezo wangu wa mashindano ya pikipiki, sikutaka tena kuhatarisha maisha yangu. Lakini sasa, nilitaka kutumia maisha yangu ili kumutukuza Yehova. Kwa hiyo, kujulikana sana, utukufu, musisimuko wa mashindano ya kutembeza pikipiki, mambo yote hayo hayakuwa tena ya maana kwangu.

Nilifikia kuelewa kwamba nina daraka mbele ya Yehova, Mutoaji wa uzima

Katika mwaka wa 1996, nilienda kwenye mukusanyiko wa kimataifa wa Mashahidi wa Yehova katika muji wa Tallinn, Estonia. Mahali tulifanyia mukusanyiko haikuwa mbali sana na uwanja ambamo nilifanyia mashindano ya pikipiki mara kwa mara. Kwenye mukusanyiko, niliona watu kutoka inchi mbalimbali wakikusanyika katika umoja na amani. Kwa mufano, wakati Shahidi mumoja alipoteza mukoba wake, niliwaza kwamba hatauona tena. Lakini, kisha muda mufupi, Shahidi mwengine alipata mukoba huo na akaurudishia dada huyo, hakuna kitu chochote kilichopotea ndani. Nilishangaa sana! Sasa nilielewa kwamba Mashahidi wa Yehova wanaishi kabisa kulingana na kanuni za juu za Biblia. Mimi na Evija tuliendelea na funzo letu la Biblia, na katika mwaka wa 1997, tulibatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA:

Wamoja kati ya marafiki wangu wamekwisha kufa kwa sababu ya maisha mabaya ya kutembeza pikipiki haraka. Kwa kujifunza Biblia, nilifikia kuelewa kwamba nina daraka mbele ya Yehova, Mutoaji wa uzima. Kwa kweli, kuelewa jambo hilo kumeokoa maisha yangu.

Kwa miaka ine, mimi na Evija tulipata pendeleo la kufanya utumishi wa wakati wote kwenye ofisi ao biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika muji wa Riga. Sasa tunafurahia kumulea binti yetu, Alise, na kumusaidia akomae akiwa mwenye kumupenda Yehova. Tena, nina pendeleo la kupitisha siku moja kila juma kwenye biro ya kutafsiri, ili kutengeneza motokari na vyombo vingine vyenye kuharibika. Ninafurahi sana kutumia vizuri ufundi mbalimbali niliojifunza nilipokuwa mutoto! Kwa kweli, ninaendelea kubomoa vitu na kuviunganisha tena.

Ninapendezwa sana na pendeleo la kutoa ushahidi juu ya Mungu wa pekee wa kweli pamoja na familia yangu, hayo yote ni kwa sababu ya mambo niliyojifunza kupitia Biblia. Kwa kweli, ahadi ya paradiso duniani ilibadilisha maisha yangu!