Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Marek M. Berezowski/Anadolu Agency via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Mwaka Moya Inaenea Tangu Vita Ianze mu Ikrene​—Ni Tumaini Gani Yenye Biblia Inatoa?

Mwaka Moya Inaenea Tangu Vita Ianze mu Ikrene​—Ni Tumaini Gani Yenye Biblia Inatoa?

 Siku ya tano, Tarehe 24 Mwezi wa 2, 2023, mwaka moya ilienea tangu jambo moya ya mubaya sana itokee, ni kusema, tangu vita ianze mu Ikrene. Kulingana na ripoti fulani, maaskari 300000 hivi wa mu Ikrene na Urusi waliuawa ao kuumia, na inakadiriwa kama raia 30000 hivi walikufa mu ile vita. Lakini, inaonekana kama hesabu ya wale wenye walikufa iko yulu zaidi ya ile.

 Jambo ya kuhuzunisha, iko naonekana kama ile vita haitaisha hivi karibuni.

  •   “Sasa ni karibu mwaka moya tangu maaskari wa Urusi walishambulia Ikrene, na hakuna alama yoyote yenye inaonyesha kama ile vita itaisha. Iko naonekana kama hakuna hata jeshi moya kati ya ile majeshi mbili yenye itapata ushindi, na hakuna hata jambo moya yenye inaonyesha kama inawezekana ile majeshi iikale pamoya juu ya kusikilizana ili kumaliza ile vita.”​—NPR (National Public Radio), Tarehe 19 Mwezi wa 2, 2023.

 Kusema kweli, watu wenye hawana kosa wako nateseka na kuumia sana juu ya ile vita na vita ingine yote yenye iko nafanyika mu dunia leo. Ni tumaini gani yenye Biblia inatoa? Kuko siku vita itaisha?

Vita yenye itamaliza vita yote

 Biblia inazungumuzia vita yenye itaokoa wanadamu, hapana kuwaua. Na inaita ile vita Armagedoni, ni kusema, “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14, 16) Kupitia ile vita, Mungu atatosha utawala wa wanadamu, wenye uko naleta vita migi sana yenye iko naua watu. Juu ya kujua namna Armagedoni italeta amani ya lote, soma habari zenye kufuata: